CANADA KUTOA SHILINGI BILIONI 2 ZA KENYA KUSAIDIA WAFANYABIASHA WADOGO NA WAKATI

Nchi ya Canada imetangaza kutoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 2 za Kenya kusaidia wafanyabiashara wadogo na wakati kupata mikopo ya kupanua biashara zao.

Waziri wa Viwanda na Biashara wa Canada ametoa kauli hiyo kando ya Mkutano wa Shirikisho la Biashara Duniani (WTO), ambapo amesema fedha hizo zitasaidia kupunguza umasikini miongoni mwa wakenya waliokwenye mikoa iliyotengwa kifedha.

Waziri huyo, Bw. Chrystia Freeland, amesema Canada itachangia dola milioni 19.5 kwa mradi huo wa kuwasaidia wafanyabiashara wadogo na wakati Kenya kwa miaka saba, hadi mwaka 2021.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni