Mkuu 
wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Dodoma,SSP Nuru Selemani  
akiwakiwaelimisha abiria ndani ya basi lilofanya safari zake mikoani 
ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni ya”Wait to Send”inayotoa elimu 
kwa madereva kutokutumia simu na kilevi wakati wote wakitumia vyombo vya
 moto.Kampeni hiyo inadhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Askari
 wa Jeshi la Polisi – Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Dodoma SGT. 
Tunu Kuta(kulia)  akimpima kiwango cha pombe mwilini dereva wa basi la 
kwenda mikoani, Masoud Seleman ikiwa ni mwendelezo wa kampeni ya”Wait to
 Send”inayodhaminiwa na Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Jeshi la 
polisi kitengo hicho katikati Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani mkoa
 huo SSP Nuru Selemani na wapili kulia ni Kaimu mkuu wa kanda ya kati wa
 Vodacom Tanzania,Heladius Kisiwani. 
Kaimu 
mkuu wa kanda ya kati wa Vodacom Tanzania,Heladius Kisiwani(kulia)akimpa
 maelezo dereva wa basi liendalo mikoani,Masoud Selemani kuhusiana na 
pete ya kidoleni inayotolewa na Kampuni hiyo kwa kushirikiana na jeshi 
la Polisi kitengo cha Usalama barabarani yenye ujumbe“Wait To Send” 
unaohamasisha madereva wa vyombo vya moto kutokutumia simu za mkononi 
wakiwa wanaendesha vyombo hivyo. Zoezi hili lilifanyika leo katika kituo
 cha mabasi yaendayo mkoani cha Dodoma.Katikati Mkuu wa Kikosi cha 
Usalama Barabarani Mkoa wa Dodoma,SSP Nuru Selemani.
Mkuu 
wa kitengo cha elimu kwa Umma kitengo cha Usalama barabarani makao makuu
 ya Polisi  ASP,Abel Swai akitoa elimu kwa abiria ndani ya basi 
liliendalo mikoani katika stendi kuu ya mabasi Dodoma ikiwa ni sehemu ya
 mwendelezo wa kampeni ya”Wait to Send”inayotoa elimu kwa madereva 
kutokutumia simu na kilevi wakati wote wakitumia vyombo vya moto.Kampeni
 hiyo inadhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Mkuu 
wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Dodoma,SSP Nuru Selemani(kulia)
 akitoa maelezo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)Kuhusiana na 
mwendelezo wa kampeni ya”Wait to Send”inayotoa elimu kwa madereva 
kutokutumia simu na kilevi wakati wote wakitumia vyombo vya moto.Kampeni
 hiyo inadhaminiwa na Vodacom Tanzania.Wengine kutoka kusho ni Meneja 
Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu na Kaimu Mkuu wa kanda ya 
kati wa kampuni hiyo Heladius Kisiwani.
Baadhi
 ya Madereva wa mabasi yanayosafirisha abiria mikoani wakimsikiliza 
Kaimu Mkuu wa kanda ya kati wa Vodacom Tanzania,Heladius Kisiwani(kulia)
 akiwapatia elimu kuhusiana na mwendelezo wa kampeni ya”Wait to 
Send”inayotoa elimu kwa madereva kutokutumia simu na kilevi wakati wote 
wakitumia vyombo vya moto.Kampeni hiyo inaendeshwa na Jeshi la polisi la
 Usalama barabarani kwa kushirikiana na Vodacom Tanzania.
Shughuli
 ikiendelea ya kutoa elimu kuhusiana na mwendelezo wa kampeni ya”Wait to
 Send”inayotoa elimu kwa madereva kutokutumia simu na kilevi wakati wote
 wakitumia vyombo vya moto.Kampeni hiyo inaendeshwa na Jeshi la polisi 
la Usalama barabarani kwa kushirikiana na Vodacom Tanzania.
Kampeni
 ya usalama barabarani ya kuwataka madereva nchini kuzingatia sheria za 
usalama barabarani,leo imefanyika katika Mkoa wa Dodoma.
Madereva
 wameendelea kuhimizwa kutotumia vinywaji vyenye ulevi na kuacha tabia 
ya kuongea na simu au kutuma na kupokea ujumbe wa maneno (sms) 
wanapokuwa wanaendesha vyombo vya moto.
Mkuu 
wa kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa Dodoma, SSP Nuru Selemani 
 amesema kampeni hii ni muhimu katika kupunguza matukio ya ajali 
“Watumiaji wa barabara hii ya mkoa wa Dodoma  ni wengi hususani madereva
 wa vyombo vya moto hawana budi kuzingatia maelekezo ambayo tumekuwa 
tukiwapa katika kampeni hizi ili tupate matokeo mazuri kwa kupunguza 
ajali kama ilivyokusudiwa”Alisema
Alisema
 madereva wakizingatia sheria za barabarani  kwa kiasi kikubwa ajali 
zinazoendelea kutokea kila siku zitapungua hususani katika kipindi hiki 
cha msimu unakoelekea wa sikukuu na aliipongeza kampuni ya Vodacom kwa 
kuunga mkono jitihada za serikali katika kupambana na tatizo hili ambalo
 limekuwa sugu.
Kwa 
upande wake,Kaimu  Mkuu wa kanda ya kati wa asoko wa Vodacom Tanzania 
Heladius Kisiwani, alisema Vodacom itaendelea  kushirikiana na serikali 
katika kuunga mkono jitihada za kuondoa  matatizo kwenye jamii kama 
lilivyo tatizo hili la ajali ili kuhakikisha wananchi wanaishi maisha 
murua na marefu.”Tunatoa rai kwa madereva wote kuzingatia sheria za 
barabarani na kutokutumia simu wakati wowote wakiwa wanatumia vyombo vya
 moto".
 Aliongeza
 kuwa Vodacom itakuwa mstari wa mbele kuelimisha jamii athari za 
kuendesha gari wakati huo huo unatumia simu  ya mkononi  kupitia kampeni
  ya "Wait to Send" pia itaendelea kuhamasisha madereva kuzingatia 
sheria za usalama barabarani.
 Alisema
 kampuni hiyo itaendeleza kutoa elimu kwa mikoa mingine pia katika 
uhamasishaji wa madereva kuzingatia sheria za barabarani katika miji ya 
Morogoro,Dar es Salaam na mikoa mingine na kampeni hizi zitaendelea 
kufanyika sehemu mbalimbali nchini.
Katika
 kampeni ya leo wafanyakazi wa Vodacom kwa kushirikiana na askari wa 
 usalama barabarani  walitoa uhamasishaji kwa madereva kuacha kuongea na
 simu wanapoendesha vyombo vya moto na kuwagawia madereva pete maalum za
 kuwatahadharisha kutotuma ujumbe wa simu za mkononi wanapokuwa 
wanaendesha vyombo vya moto pia zoezi la kupima madereva kubaini kama 
wanatumia vilevi lilifanyika ambapo wadereva waliokutwa wanaendesha 
vyombo vya moto walichukuliwa hatua kali za kisheria.
Baadhi
 ya abiria walioshuhudia kampeni hii mkoani Dodoma wamesema ni ya muhimu
 itasaidia kupunguza ajali nchini.”Hivi sasa ajali nyingi zinazotokea 
hapa nchini zinasababishwa na uzembe wa madereva,kampeni hizi 
zikiendelea zitapunguza ajali kwa kiasi kikubwa”.Alisema Sunday Israel 
mkazi wa Dodoma aliyekuwa safarini kuelekea Singida.







Hakuna maoni:
Chapisha Maoni