MALALA ASEMA KAULI YA DONALD TRUMP INACHOCHEA UGAIDI

Mshindi wa tuzo ya Nobel Malala Yousafzai amemlaumu mtia nia ya urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican, Donald Trump, kwa kauli yake ya kutaka waislamu wasiruhusiwe kuingia Marekani.

Malala ambaye alipigwa risasi ya kichwa na Wataliban kwa kutetea elimu ya mtoto wa kike, amesema matamshi hayo ya Trump yalijaa chuki, na kuwashutumu waislam wote kwa ugaidi, kutachochea idadi ya waislam wanaojiunga na ugaidi.

Malala alikuwa akiongea katika tukio la maadhimisho tangu kufanyika shambulizi la wapiganaji wa Taliban katika shule moja huko, Peshawar, Pakistan na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 140, wengi wao wakiwa watoto.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni