MTUHUMIWA WA MAUAJI YA MFANYAKAZI WA TANAPA AKAMATWA

Image result for picha za kamanda sabas
Na Mahmoud Ahmad Arusha
 Jeshi la polisi mkoani hapa limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa wa mauaji ya mfanyakazi wa shirika la hifadhi za taifa,na mkuu wa Taarifa Fiche wa shirika hilo Emily Kisamo aliyeuwawa mwishoni  mwa wiki katika eneo la Kikwakwaru Kata ya Themi jijini Arusha.

Akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwa kwake jijini hapa Kamanda wa jeshi la polisi mkoani hapa Liberatus Sabas alisema jeshi hilo limefanikwa kumkamata mtu anayeitwa Ismail Swalehe Sang’wa 20 mtunza bustani mkazi wa Sepuka Wilayani Ikungi mkoani Singida.

Alisema kuwa siku ya tukio mtuhumiwa alimvizia marehemu akinywa uji Sebuleni na kumkata shingoni kwa kutumia kitu chenye ncha kali,baada ya kukamatwa mtuhumiwa aliweza kueleza jinsi alivyotekeleza mauaji hayo huku akieleza pia sababu za kufanya hivyo ni tama ya pesa alizokuwa nazo marehemu hapo kiasi cha tsh. Million 5.

Kamnda Sabas aliendelea kusema kuwa baada ya kufanya mauaji hayo mtuhumiwa alikiri kwamba alianza usafi wa ndani ya nyumba kwa kupiga deki na kasha kulisafisha gari kwa nje na kuliendesha mpaka eneo alipolitelekeza gari la marehemu Kisamo.

Mara baada ya upekuzi polisi waligundua vitu kadhaa kwenye gari hilo vikiwemo fedha taslimu kiasi cha Tsh.Milion 4.29,4000,simu za mkononi tatu. Aina ya Samsung,na vocha aina ya Vodacom za 5000 zenye thamani ya 70000 vyote hivyo vilifukiwa kwenye banda la kuku.
Pia polisi waligundua panga moja lililokuwa na damu ambalo lilikutwa stoo na vitu vingine kama taulo kubwa nne,kitambaa cha mezani,suruali moja ya mtuhumiwa ambazo zilifichwa kwenye migomba karibu na mabanda ya kuku na zilikuwa na damu ambapo ndizo zilitumika na myuhumiwa kupigia deki ndani baada ya kumuua marehemu.

Kamanda alisema kuwa kufuatia tukio hilo jeshi la polisi mkoani hapa linaendelea na upelelezi na pindi utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Wakati huo huo jeshi la polisi liemsema kuwa limejipanga kuhakikisha wakazi wa mkoa huo wanasherehekea sikukuu zote Maulid na Krismas kwa amani na utulivu na kuwataka wakazi wote kuhakikisha hawafanyi vitendo vyovyote vinavyoashiria uvunjifu wa amani.

Kamanda wa jeshi Hilo mkoani hapa Liberatus Sabas pia akawatakiwa wakazi hao sikukuu njema na yenye Baraka itakayoendana na kukukaribisha mwaka bila ya kuvunja sheria za nchi na kufanya matukio ya fujo na kushrehekea kwa amani sikukuu hiyo
Mwisho……………………………………………..

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni