Ofisa 
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha 
Kazaura (kushoto) na Ofisa Ufundi (IT) wa kampuni hiyo, Rehema Maswanya 
(kulia) kwa pamoja wakifungua pazia kuashiria uzinduzi wa teknolojia ya 
4G LTE iliyozinduliwa leo jijini Dar es Salaam. 
Ofisa 
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha 
Kazaura (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu 
ya uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE inayotolewa na kampuni hiyo. Kushoto
 ni Ofisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya TTCL, Peter Ngota akiwa 
katika mkutano huo. 
Ofisa 
Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya TTCL, Peter Ngota (kushoto) 
akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) katika hafla 
ya TTCL kuzinduwa teknolojia ya 4G LTE iliyofanyika leo jijini Dar es 
Salaam. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania 
(TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura. 
Ofisa 
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha 
Kazaura (kushoto) na Ofisa Ufundi (IT) wa kampuni hiyo, Rehema Maswanya 
(kulia) kwa pamoja wakifungua pazia kuashiria uzinduzi wa teknolojia ya 
4G LTE iliyozinduliwa leo jijini Dar es Salaam. 
Uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE toka TTCL leo. 
Kulia 
ni wataalamu wa huduma ya teknolojia ya 4G LTE kutoka TTCL wakitoa 
ufafanuzi kwa baadhi ya wageni waalikwa walioshiriki katika hafla ya 
uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE. 
Kulia 
ni wataalamu wa huduma ya teknolojia ya 4G LTE kutoka TTCL wakitoa 
ufafanuzi kwa baadhi ya wageni waalikwa walioshiriki katika hafla ya 
uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE. 
Kushoto
 ni wataalamu wa huduma ya teknolojia ya 4G LTE kutoka TTCL na maofisa 
waandamizi wakitoa ufafanuzi kwa baadhi ya wageni waalikwa walioshiriki 
katika hafla ya uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE. 
KAMPUNI
 ya Simu nchini Tanzania (TTCL) leo imezinduwa mtandao unaotumia 
teknolojia ya 4G LTE unaoanza kutoa huduma jijini Dar es Salaam. Mtandao
 huo wenye teknolojia mpya na ya kisasa wenye kasi kubwa utatoa huduma 
katika maeneo 11 ambayo ni pamoja na Uwanja wa Ndege wa Mwalimu J.K. 
Nyerere, Pugu Road, Posta Mpya, Upanga, Kinondoni, Ubungo, Oysterbay, 
Mwenge, Mbezi Tangibovu, Mbezi Exchange, Kunduchi Salasala, na Wazi 
Tegeta.
Akizungumza
 leo jijini Dar es Salaam wakati akizinduwa rasmi teknolojia hiyo, Ofisa
 Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura alisema licha ya kuzinduwa
 huduma hiyo katika maeneo 11 kwa sasa mafundi wa kampuni hiyo wapo 
kazini wakiendelea na awamu ya pili ya kufunga mitambo ili huduma hiyo 
itolewe pia katika maeneo mengine 14 ya jiji la Dar es Salaam.
Aliyataja maeneo mengine ambayo mitambo inaendelea kufungwa kwa sasa 
kuwa ni pamoja na Kigamboni, Masaki, Temeke, Kimara, Jangwani, Kariakoo,
 Chuo Kikuu, Kurasini, Mbezi Chini Gongo la Mboto, Tabata, Kibamba, 
Kongowe na Bunju.
"...Awamu ya pili ya mradi huu itakuwa imekamilisha maeneo yaliyobaki
 ya mkoa wa Dar es Salaam na pia kupeleka mawasiliano hayo katika mikoa 
mingine ikiwa ni pamoja na Arusha, Mwanza, Mbeya, Dodoma na kwingineko,"
 alisema Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kazaura.
Alisema uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE unakuwa umekamilisha nia ya 
siku nyingi ya kampuni ya TTCL ya kuwahudumia wateja katika nyanja zote 
za mawasiliano (Fixed-mobile convergence) kwa kutumia teknolojia ya simu
 za mezani na simu za mkononi.
Akifafanua zaidi Dk. Kazaura alisema uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE
 utakuwa na mchango mkubwa katika kukuza na kuongeza kasi ya shughuli za
 maendeleo ya kijamii na kiuchumi, kuchangia katika kukuza teknolojia ya
 habari na mawasiliano na pia kuongeza uzalishaji kwenye sekta 
mbalimbali za maendeleo.
Aidha aliongeza kuwa TTCL inaamini mtandao wa 4G LTE utafungua fursa 
pekee katika kukuza sekta ya elimu nchini kwa njia ya mtandao (E 
education). Na pia ubora wa huduma hiyo ya intaneti utatoa fursa kwa 
wanafunzi, wakufunzi, wataalam, wanazuoni na walimu kutumia teknolojia 
katika kujifunza mambo mbalimbali ya kitaaluma na nje ya taaluma.
Kwa upande wake Ofisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya TTCL, 
Peter Ngota akifafanua zaidi kwa wanahabari alisema mtandao wa 4G LTE 
utaongeza fursa katika sekta ya afya ambapo hospitali, vituo vya afya, 
vyuo vya afya na wadau mbalimbali wataweza kutumia mtandao huo katika 
kuongeza ufanisi wa kutoa huduma bora za afya kwa wananchi tena kwa 
haraka zaidi.
Alisema
 mtandao huo pia utazinufaisha sekta nyingine za kiuchumi kama vile 
sekta ya biashara, viwanda, kilimo na nyinginezo. "...Wafanyabiashara na
 wazalishaji wa bidhaa wanahitaji mawasiliano ya uhakika katika shughuli
 zao. Mtandao huu wa 4G LTE utakuwa mkombozi wao na utaleta mageuzi 
katika kuongeza uzalishaji, kupanua wigo wa masoko ya bidhaa kwa 
wakulima, masoko kwa wajasiliamali, masoko kwa makampuni ndani na nje ya
 mipaka ya Tanzania," alisema Peter Ngota.
Hata hivyo, Ngota aliongeza kuwa uzinduzi huo unaenda sambamba na 
uboreshaji vifurushi rafiki vya intaneti kwa wananchi hivyo kuwaomba 
wananchi kuiunga mkono kampuni ya kizalendo ya TTCL katika kuboresha 
huduma za mawasiliano nchini.








Hakuna maoni:
Chapisha Maoni