Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu 
wenye Ulemavu), Mhe. Bibi Jenista Mhagama (Mb), akiangalia Sehemu ya 
mtaro wa maji katika eneo la Tegeta, Basihaya wilayani Kinondoni, Jijini
 Dar es Salaam leo wakati alipofanya ziara kuangalia jinsi wilaya hiyo 
ilivyojiandaa kukabili maafa ya Mvua zinazoendelea kunyesha jijini humo,
 kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda. 
 Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu 
wenye Ulemavu), Mhe. Bibi Jenista Mhagama (Mb), akimsikiliza mkazi wa 
Tegeta, Basihaya Jijini Dar es Salaam, Jumanne Malongo alipokuwa 
akimueleza jinsi wembamba wa mtaro huo unavyosababisha maji kujaa katika
 makazi yao, leo wakati alipofanya ziara kuangalia jinsi wilaya hiyo 
ilivyojiandaa kukabili maafa ya Mvua zinazoendelea kunyesha jijini humo,
 kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda. 
 Kaimu
 Mkurugenzi Halmashauri ya Manisipaa kinondoni, Ando Mwakunga akimueleza
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge; Kazi, Ajira, Vijana 
na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Bibi Jenista Mhagama (Mb), uharibifu wa 
“kalvati” katika eneo la Boko, Ununio Jijini Dar es Salaam, leo wakati 
Waziri huyo alipofanya ziara kuangalia jinsi wilaya hiyo ilivyojiandaa 
kukabili maafa ya Mvua zinazoendelea kunyesha jijini humo. 
 Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu 
wenye Ulemavu), Mhe. Bibi Jenista Mhagama (Mb), akiteta na Mkurugenzi 
Idara ya Uratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Brig. Jen, Mbazi Msuya juu 
ya ujenzi wa mtaro wa maji katika eneo la Mnyamani, Buguruni wilayani 
Ilala, Jijini Dar es Salaam leo wakati alipofanya ziara kuangalia jinsi 
wilaya hiyo ilivyojiandaa kukabili maafa ya Mvua zinazoendelea kunyesha 
jijini humo. 
Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu 
wenye Ulemavu), Mhe. Bibi Jenista Mhagama (Mb), akitoa maelekezo baada 
ya kutoridhishwa na ujenzi wa mtaro wa maji katika eneo la Mnyamani, 
Buguruni Ilala Jijini Dar es Salaam, kwa Uongozi wa Halmashauri ya 
Manispaa hiyo kumpatia taarifa ndani ya siku tano inayoeleza ni jinsi 
gani watakavyokamilisha ujenzi huo, leo wakati alipofanya ziara 
kuangalia jinsi wilaya hiyo ilivyojiandaa kukabili maafa ya Mvua 
zinazoendelea kunyesha jijini humo.
 (Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni