MWANDISHI WA HABARI MAREHEMU DOTO MZAVA AZIKWA KIJIJINI KWAO VUDEE SAME MKOANI KILIMANJARO.

Wazazi wa marehemu Doto Mzava wakitoa heshima za mwisho kwa mtoto wao mpendwa.
Baadhi ya wanandugu na marafiki wakitoa heshima za mwisho .
Baadhi ya marafiki ,ndugu na majirani waliotoka maeneo mbalimbali kushiriki maziko ya marehemu Doto
Jeneza lenye mwili wa marehemu Doto likitolewa ndani ya nyumba .
Mmoja wa wakurugenzi wa Jamii Media group Maxence Melo alikua miongoni mwa waombolezaji katika mazishi ya mmoja wa wafanyakazi wake wa mtandao wa Jamii Forum.
Hali ya Majonzi ilitawala nyumbani hapo
Mchungaji wa kanisa la Adventista Wasabato ,Mchungaji Ezekiel akiongoza ibada ya mazishi ya marehemu Doto.
Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Marehemu Doto tayari kwa ajili ya kuwekwa kwenye nyumba yake ya milele.
Jeneza likishushwa kaburini.
Mchungaji Ezekiel akisoma neno mbele ya kaburi.
Mchungaji akiweka mchanga kaburini. 
zoezi la kufukia kaburi likaanza .
Baadhi ya waombolezaji wakiwa katika maziko ya marehemu  Doto kijijini Vudee wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro.
Mmoja wa wakurugenzi wa Jamii Media group Maxcence Melo akizungumza kwa niaba ya Mtandao wa wamiliki na wapasha habari kwa njia ya Mtandao Tanzania , TBN  na Jamii Forum ambako marehemu alikua akifanya kazi.
Mmoja wa Wanachama wa kundi la Mtandao la MADA MOTO la mjini Moshi ,Charles Ndagula akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya kundi hilo ambalo Doto alikuwa mwanachama wake.
Kiongozi wa kundi la Prince Media akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya wanachama wa kundi hilo ambao walisoma na marehemu  Doto.
Mweka hazina wa Arusha Press Club (APC) Pamela Mollel akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya wanahabari wa mkoani Arusha
Salamu za Rambi rambi zilitoka maeneo mbalimbali.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni