HALMASHAURI YAVUNJA NDOA BUBU NA KURUDISHA WANAFUNZI SHULENI LONGIDO


Image result for watoto wanaokeketwaNa Mahmoud Ahmad Arusha
HALMASHAURI ya wilaya ya Longido,mkoani Arusha, imefanikiwa kuvunja ndoa bubu na kuwarejesha wanafunzi wawili wa shule ya msingi walioachishwa shule na kuolewa na kuwarejesha shuleni na kuendelea na masomo yao mwaka 2015 .

Afisa elimu wa halmashauri ya wilaya ya Longido, Shaaban Shemzighwa, ameyaeleza hayo kwenye kikao cha elimu cha mkoa kilichokuwa kikipitisha majina ya wanafunzi waliohitimu elimu ya msingi mwaka 2015,ambao wamechaguliwa kujiunga na sekondari mwakani .

Akitoa ufafanuzi wa hoja za wajumbe ambao walitaka kufahamu mkakati wa halmashauri hiyo kukabiliana na utoro unaosababsha wanafunzi hasa  wasichana ambao wamekuwa wakiacha shule na kuolewa ,amesema halmashauri inaendelea na kuwarejesha wanafunzi wote waliotoroka na kuolewa.

Amesema wanafunzi wawili ambao walikuwa wameolewa wamerejeshwa kuendelea na masomo yao katika shule ya msingi Kitumbeine na lengo ni kukabiliana na utoro wa wanafunzi.

Amesema licha ya utoro huo wa wanafunzi bado halmashauri hiyo ya Longido, imezidi kaulisha wanafunzi wengi ukilinganisha na halmashauri zingine za mkoa wa Arusha na hayo ni mafanikio makubwa.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya hiyo Ernest Kahindi, akichangia kwenye kikao hicho amesema watoto wa jamii za wafugaji waishio maeneo yote ya mpaka na nchi ya Kenya, wanasoma shule za Kenya.

Amesema watoto wa jamii za wafugaji kusoma nchini Kenya ni jambo la kawaida na lbda inachangiwa na jamii hizo kutokuishi karibu na shule  hivyo inakuwa ni rahisi kuwapeleka nchini humo kusoma.

Amesema jiografia ya wilaya za mipakani hasa kwenye jamii za wafugaji nayo ni tatizo maeneo mengi hayana bara bara, mawasiliano ,shule wala miundo mbinu  na matokeo yake ni kuwepo na mahudhurio hafifu shuleni.
Amesema wakati wa likizo watoto hao hupelekwa nchini Kenya ambako huwa baadhi yao wanaolewa na hilo ni njambo la kawaida kwa jamii za wafugaji waishio mipakani .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni