Katibu
 Mkuu wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akizungumza
 na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kabla ya kufungua 
mkutano wa siku moja wa baraza hilo unaofanyika katika Ukumbi wa Jeshi 
la Magereza, Ukonga, jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto meza kuu ni 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, John Mngodo, kushoto ni Mwenyekiti wa 
Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) tawi la Wizara ya 
Mambo ya Ndani ya Nchi, Obeid Mbaga. Wapili kulia ni Katibu wa Baraza 
hilo, Amani Mashaka, anayefuata ni Katibu Msaidizi wa Baraza hilo, 
Jenita Ndone. Katika kikao hicho Abdulwakil aliwataka watumishi wa 
wizara yake wafanye kazi kwa uadilifu na weledi ili kuleta mafanikio 
ndani ya wizara hiyo muhimu katika maendeleo ya nchi.
Katibu
 Mkuu wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (katikati),
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, John Mngodo (wapili kushoto), 
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) tawi
 la Wizara hiyo, Obeid Mbaga. Wapili kulia ni Katibu wa Baraza hilo, 
Amani Mashaka, anayefuata ni Katibu Msaidizi wa Baraza hilo, Jenita 
Ndone wakiwaongoza wajumbe wa Baraza hilo kuimba wimbo wa mshikamano 
daima kabla ya Katibu Mkuu kufungua kikao hicho kilichofanyika katika 
Ukumbi wa Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
 wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) tawi la Wizara
 ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Obeid Mbaga akimkaribisha mgeni rasmi ambaye
 ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil (kulia) kuja 
kuzungumza na wajumbe wa kikao hicho (hawapo pichani) kabla ya kufungua 
rasmi kikao hicho. Kushoto meza kuu ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,
 John Mngodo. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa 
Magereza, Ukonga jijini Dar es Salaam. 
Mtoa 
Mada wa Benki ya NMB, Faraja Kaziulaya akiwasilisha mada ya jinsi 
wanavyotoa huduma zao pamoja na bidhaa mbalimbali zinazotolewa na Benki 
hiyo, wakati wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya 
Ndani ya Nchi kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Magereza, 
Ukonga jijini Dar es Salaam. 
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (meza ya 
mbele kulia), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, John Mngodo wakiwa na 
baadhi wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo, wakimsikiliza 
kwa makini mtoa Mada wa Benki ya NMB, Faraja Kaziulaya (hayupo pichani) 
akiiwasilisha mada ya jinsi wanavyotoa huduma zao pamoja na bidhaa 
mbalimbali zinazotolewa na Benki hiyo. Abdulwakil alifungua kikao cha 
Baraza hilo na wajumbe walijadili masuala mbalimbali ya kuiendeleza 
Wizara hiyo zaidi. 
Mjumbe
 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kutoka 
Zanzibar, Shemsa Said akichangia mada katika kikao cha Baraza hilo 
kinachofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Magereza, Ukonga jijini Dar 
es Salaam. 
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil (wanne 
kushoto waliokaa), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, John Mngodo (watatu
 kushoto waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la
 wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ukonga jijini Dar es 
Salaam. Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano-MOHA.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni