Baadhi
 ya waraghabishi wa kijiji cha Nyandekwa Wilayani Kahama wakiongea na 
waandishi wa habari waliofika kijijini hapo kwa ajili ya kujionea 
matokeo mbali mbali baada ya waraghabishi kuwasaidia wananchi hao 
kuchukua hatua katika kila jambo kwa maendeleo ya kijiji chao.
Mdau Krantz
 Mwantepele akihoji maswali kwa Dada Miriam Stefano (Aliyejishika tama )
 ambaye amekuwa mchango mkubwa kwa kutoa elimu ya uzazi na mabadilko ya 
mwili kwa vijana wa kike katika baadhi ya shule za sekondari na msingi 
katika kijiji hicho. 
Picha 
ya pamoja nikiwa na waraghabishi wa kijiji cha Nyandekwa Wilayani na 
waandishi wa habari tuliopata bahati ya kutembelea kijiji hicho na 
kujifunza namna gani wameweza kuwa chachu ya maendeleo katika kijiji 
hicho.
Na Krantz Mwantepele ,KAHAMA
Mkutano
 mkuu wa Kijiji cha Nyandekwa wilayani Kahama mkoani Shinyanga 
uliofanyika mwishoni wa mwezi wa tisa umeazimia kuwashikinikiza wazazi 
wa kijiji hicho kuwapeleka watoto wao shule Azimio hilo Pia limeelekezwa
 kwa vijana wanaokaa vijiweni kuwataka kushirki katika shughuli 
mbalimbali za kiuchumi na sio kukaa vijiweni pia kushiriki katika 
mikutano mbali mbali ya kijiji kujua maendeleo ya kijiji Iikihusisha 
mapato na matumizi. 
Mkutano
 huo umepitisha maazimio matano yanayolenga kurejesha nidhamu Na heshima
 kijijini Nyandekwa hatua hiyo imefikiwa Kutokana Na wananchi wa kijiji 
hiki kutoona umuhimu wao kuchukua hatua za kujikwamua kiuchumi na pia 
Kuwa na ujasiri wa kuhoji mapato na matumizi kwa ajili ya kijiji chao.
Hali 
hiyo inatokana na juhudi za dhati bila kukata tamaa zilizofanywa 
waraghabishi na watetezi wa haki za binadamu wa kijiji hicho akiwemo 
Miriam Stefano, Boniface Izengo , Matilda Peter ,Na Mwenyekiti Wa 
kitongoji cha Busolwa Bi Ana Alphonce kuwapa ujasiri na elimu ya uraia 
wananchi wenzao ili wawe chachu ya maendeleo.
Kwa 
mujibu wa bi Anna Alphonce ambaye pia ni mwenyekiti wa kitongoji cha 
Busolwe aliweza kuongea na mtandao wa Mwanaharakati Mzalendo Blog 
alisema kupitia mikutano mbalimbali ya kijiji aliweza kutoa hamasa kwa 
wanawake na wanaume wa kijiji hicho kushiriki katika uchaguzi mkuu 
uliopita katika kusikiliza sera za viongozi na mwishowe kushiriki kupiga
 kura.Na kwa muda mfupi aliweza kufanikisha wanawake wengi kushiriki 
katika maamuzi ya kijiji pia kuwa na ujasiri wa kuhoji katika mikutano 
ya kijiji.
Wengi 
wa wanakijji ambao wamekuwa waraghabishi katika kijiji hiki waliweza 
kupata mafunzo haya ya uraghabishi ambapo waliweza kujua baadhi ya haki 
zao na kuwa na uajasiri wa kuhoji mapato na matumizi ya kijiji hicho 
ambapo mwanzoni walikuwa hawapati fursa hiyo kwa wakati .Waraghabishi 
hawa wamekuwa chachu ya maendeleo ya kijiji cha Nyandekwa katika sekta 
za kiuchumi ,kisiasa na kijamii kwa kuwaelimisha wanakijiji wenzao haki 
na wajibu wao kwa nafasi kubwa .
“Viongozi
 wa kijiji hiki hawakuweza kutupa mrejesho wa kila jambo linalofanyika 
kwa kijiji hcetu hasa katika mikutano ya kijiji na sisi tulipoanza 
kuhoji tulikosa ushirikiano kwao lakini mwishowe wananchi wengi waliona 
umuhimu wa kushirikishwa” alinukuliwa bw. Boniface Izengo mmoja wa 
waraghabishi wa kijiji hiki alipokuwa akiongea na mwandishi wa habari 
hii.
Katika
 hatua nyingine mmoja wa waraghabishi wa kijiji hiki bi Matilda Peter 
amekuwa ni mmoja wa vijana wanaotoa elimu ya uzazi wa mpango kwa makundi
 rika ambapo hukutana na vijana hasa wanafunzi wa shule ya msingi na 
sekondari na kuwajuza kuhusu mabadiliko ya mwili yao na pia kuwashauri 
jinsi ya kuepuka maambukizi magonjwa ya ngono na mimba zisizotarajiwa.
Maazimio
 yaliyopitishwa kuwa ni vijana wanaokaa au kusimama ovyo barabarani na 
maeneo mengine bila shughuli maalum kuwajibishwa na pia kuweza 
kuwawezesha kuwashirikisha katika shughuli za kijiji hicho ikiwemo 
kushiriki katika shughuli mbalimbali za uzalishaji kijijini hapo
Pia 
mkutano wa kijiji hiki uliazimia kuwa mapato na matumizi kuweza 
kujadiliwa kwa uwazi na pia kubandikwa katika mbao za matangazo hapo 
kijijini kuwezesha wananchi hao kuweza kusoma na kuelewa kila 
kinachoendelea kijijini kwao katika swala la maendeleo ya uchumi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni