Na Mwandishi wetu,Mbeya,Jamiimojablog
Katika hali isiyokuwa ya kawaida mwanaume mmoja Mkazi wa kijiji cha Malolo Ndugu Chipunguli Mkisi (30)
 amemuua mke wake kwa kumkata panga kichwani kisha yeye mwenyewe kujiua 
kwa kujinyonga.
Akizungumzia tukio hilo 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ndugu Ahmed Msangi amesema 
tukio hilo la aina yake limetokea Desemba mwaka huu majira ya saa 7 
mchana huko katika kijiji cha Malolo, Kata ya Msia, wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Mbeya.
Msangi amemtaja mwanamke
 huyo kuwa ni Neva Mwaweza (24) Mkazi wa Malolo ambaye 
ameuwawa na mumewe kwa kukatwa kichwani .
Kamanda
 Msangi amesema chanzo cha tukio 
hilo ni wivu wa kimapenzi baada ya mwanaume kumtuhumu mke wake kuwa na 
mahusiano ya kimapenzi na mwanaume mwingine. Inadaiwa kuwa baada ya 
tukio, mtuhumiwa alijinyonga kwa kutumia kamba kwenye mti umbali wa mita
 100 kutoka nyumbani kwake. 
Aidha
 mwili wa marehemu [mwanaume] ulikutwa ukiwa na majeraha kwenye vidole 
na kando kukiwa na panga na alikutwa na ujumbe uliokuwa na maneno kuwa 
ameamua kumuua mke wake na yeye kujinyonga kutokana na mke wake kuwa na 
mahusiana ya kimapenzi na mwanaume mwingine aitwae kilasi nzowa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni