RAFIKI WA WANDANDOA WALIOFANYA MASHAMBULIZI SAN BERNARDINO AFUNGULIWA

Rafiki mmoja wa wandandoa waliofanya mashambulizi San Bernardino amefunguliwa mashtaka ya kuhusika na mauaji ya kutumia risasi ya watu 14.

Mtu huyo Enrique Marquez, miaka 24 anakuwa mtu wa kwanza kufunguliwa mashtaka kwa kuhusika na mashambulizi hayo mabaya ya kigaidi tangu tukio la Septemba 11.

Bw. Marquez amefunguliwa mashtaka kupanga mashambulizi ya kutumia bunduki na Syed Farook kwenye chuo kimoja mwaka 2011 na 2012.

Pia anashtakiwa kwa kununua kinyume na sheria bunduki mbili aina ya rifles zilizotumiwa kwa mauaji na Farook na Tashfeen Malik.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni