Afisa 
Elimu Vifaa na Takwimu Halmashauri ya Kibaha Vijijini Doris Semkiwa 
ambaye anamwakilisha Afisa Elimu wa Halmashauri ya Kibaha Vijijini 
akitoa mada kwa Washiriki wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Walimu na 
Wanafunzi katika Ufundishaji na Ujifunzaji kwa shule za sekondari (STEP)
 wakifuatilia mafunzo hayo katika kituo cha Shule ya sekondari 
Kilangalanga iliyopo wilayani Kibaha Vijijini mkoani Pwani.
Washiriki
 wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Walimu na Wanafunzi katika Ufundishaji 
na Ujifunzaji kwa shule za sekondari (STEP) wakifuatilia mafunzo hayo 
katika kituo cha Shule ya sekondari Kilangalanga iliyopo wilayani Kibaha
 Vijijini mkoani Pwani.
Washiriki
 wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Walimu na Wanafunzi katika Ufundishaji 
na Ujifunzaji kwa shule za sekondari (STEP) ambao wanafundisha somo la 
Biolojia wakitafuta baadhi ya sampuri za kufundishia somo hilo kulingana
 na mazingira waliopo. Mafunzo hayo ni ya siku tano kuanzia Tarehe 
Disemba 19 hadi 23, 2015 katika kituo cha Shule ya sekondari 
Kilangalanga iliyopo wilayani Kibaha Vijijini mkoani Pwani.
Baadhi
 ya sampuri zilizokusanywa na washiriki wa mafunzo ya kuwajengea uwezo 
Walimu na Wanafunzi katika Ufundishaji na Ujifunzaji kwa shule za 
sekondari (STEP) kwa ajili ya kufundishia la Biolojia kulingana na 
mazingira waliopo.
(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO).
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Walimu
 nchini wametakiwa kuwa wazalendo kwa kuhakikisha wanawafundisha 
wanafunzi katika muda waziada ili kuwaongezea uwezo wa ufaulu katika 
mitihani yao.
Kauli 
hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na 
Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba 
wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo Walimu na wanafunzi katika 
ufundishaji na Ujifunzaji kwa shule za sekondari (STEP) yanayoendelea 
katika mikoa sita nchini.
Aidha,
 Bw. Samataba aliwataka walimu wasihangaike kutafuta michango kwa ajili 
ya uendeshaji wa shule na badala yake wajikite katika kufundisha na 
kuwasaidia wanafunzi kupata elimu na kufaulu masomo yao kwa kuwa 
Serikali ndiyo itafanyakazi ya kuhakikisha fedha za uendeshaji wa shule 
na vifaa vinapatikana kwenye shule zote za Serikali nchini.
Mafunzo
 hayo ni ya siku tano (5) ambayo yanashirikisha walimu wa shule za 
sekondari wapatao 2,528 yameanza kufanyika kuanzia Desemba 19, 2015 na 
yanatarajia kumalizika Desemba 23, 2015.
Mafunzo
 hayo yanayolenga kuwajengea uwezo walimu na wanafunzi katika 
ufundishaji na ujifunzaji yanafanyika kwa awamu ambapo katika awamu ya 
pili yanafanyika katika mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Iringa, Singida 
na Katavi na hatimaye kufanyika katika mikoa yote nchini.
Katika
 awamu ya kwanza ya mafunzo ya  STEP  iliyofanyika mwezi Juni, 2015 
ilishirikisha mikoa ya Mwanza, Dodoma, Geita, Mara, Simiyu, Shinyanga na
 Tanga ambapo walimu wa sekondari wapatao 3,880 walipatiwa mafunzo hayo.
Katika
 kila awamu ya mafunzo, walimu wane wa masomo ya Kiswahili, Hisabati, 
Biolojia na Kiingereza kutoka kwenye shule za sekondari katika 
Halmashauri na Mkoa husika wanashiriki katika mafunzo katika vituo 
mbalimbali vinavyoandaliwa na mikoa husika.
Katika
 mafunzo hayo, walimu wanajengewa uwezo wa kuwawezesha kuwatambua 
wanafunzi wenye uwezo mdogo kimasomo na walio katika hatari ya kufeli 
mitihani ya Taifa kwa kuwapatia mafunzo rekebishi kwa lengo la 
kuwawezesha kufaulu mitihani yao.
Mafunzo
 yanayotolewa ni sehemu ya utoaji wa mafunzo ya walimu kazini ikiwa ni 
utekelezaji wa Programu ya kuboresha taaluma ya Walimu na Wanafunzi wa 
shule za Sekondari ambayo ni mojawapo ya Mpango wa Tekeleza kwa Matokeo 
Makubwa Sasa (BRN).
Programu
 ya STEP ilibuniwa na Serikali kwa lengo la kubadilisha hali ya kushuka 
kwa ufaulu wa wanafunzi na kuboresha kiwango cha ufaulu kwa kuwawezesha 
walimu kujenga tabia ya kuwatambua wanafunzi wenye uwezo mdogo kimasomo 
na walio katika hatari ya kufeli Mtihani wa Taifa kwa kuwasaidia kufanya
 Mafunzo Rekebishi.
Ili 
kuyafanya mafunzo ya nayotolewa kufanyika kwa ufanisi, Ofisi ya 
Rais,TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi 
imeandaa miongozo ya masomo husika unaotumika kuwafundishia walimu hao.
Mafunzo
 ya STEP yanatekeleza azma ya Serikali chini ya mpango wa BRN unaolenga 
kuweka mfumo thabiti wa kusimamia, kufuatilia na kutathmini mipango yake
 hususan Mpango wa Kupunguza na Kuondoa Umaskini Tanzania (MKUKUTA) na 
Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano.
BRN ni
 mfumo ambao umejikita katika kuweka vipaumbele, kufanya ufuatiliaji 
makini na uwajibikaji katika kuleta matokeo tarajiwa, Elimu ni mojawapo 
wa sekta za kipaumbele katika utekelezaji wa BRN nchini.
Sekta 
ya Elimu inavipaumbele tisa (9) vilivyoainishwa ambavyo ni upangaji wa 
shule kwa ubora wa ufaulu katika matokeo ya mitihani ya kumaliza elimu 
ya msingi na sekondari kidato cha nne, utaratibu wa utoaji tuzo kwa 
shule zinazofanya vizuri ilikuzipamotisha wa kuendelea kufanya vizuri, 
kuandaa kiongozi cha kuimarisha utendaji wa shule na kutoa mafunzo kwa 
wakuu wa shule na kufanya upimaji wa stadi za Kuandika, Kusoma na 
Kuhesabu (KKK) kitaifa.
Maeneo
 mengine ya vipaumbele katika sekta ya elimu ni pamoja na kutoa mafunzo 
ya Ufundishaji wa KKK kwa walimu wa darasa la kwanza na pili, kujenga 
uwezo wa Walimu na wanafunzi katika Ufundishaji na Ujifunzaji, Ujenzi wa
 Miundombinu muhimu ya shule, Utoaji wa Ruzuku ya Uendeshaji na Motisha 
kwa walimu.






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni