Meza kuu,wa kwanza kulia ni 
Meneja wa redio PANGANI FM Maimuna Msangi, wa pili kutoka kulia ni 
Mkurugenzi wa shirika la UZIKWASA ambalo limeratibu tamasha hilo VERA 
PIEROTH,wa tatu ni Kaimu mgeni Rasmi ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya 
Jamii Wilaya ya PANGANI Bi Patricia, na wanne ni Mratibu wa masuala ya 
UKIMWI wilaya ya PANGANI.
Mkurugenzi wa shirika la 
UZIKWASA, VERA PIEROTH akizungumza jambo wakati wa kuwakaribisha 
wananchi wa PANGANI katika tamasha hilo.
Na Mwandishi wetu
Shirika lisilo la kiserikali 
Wilayani Pangani la UZIKWASA linalojishughulisha na kuziwezesha kamati 
za kudhibiti Ukimwi, VMACK limezawadia kamati bora za kudhibiti ukimwi 
Wilayani humo.
Sherehe hizo zimefanyika sanjari na kuwazawadia kijana bora mfano wa kuigwa na mama bora mfano wa kuigwa.
Katika sherehe zilizofanyika kijiji 
cha Jaira,K ata ya Madanga wilayani Pangani na kuhudhuriwa na watu 
mbalimbali wakiwemo wananchi na viongozi kutoka halmashauri ya Wilaya ya
 Pangani mgeni rasmi alikuwa Kaimu Afisa Maendeleo Wilaya ya Pangani, 
Bi.Patricia Kinyange.
Akizungumza katika hadhara hiyo Bi. 
Kinyange amelipongeza shirika hilo kwa kuzijengea uwezo kamati hizo 
ambazo zinafanya kazi kubwa kwa jamii.
“Kwa kweli shirika la UZIKWASA 
nawapongeza sana, mnafanya kazi kubwa kwenye jamii ya Pangani na 
kwakweli watu wa Pangani wanapaswa kujivunia uwepo wenu. Nimeshangaa 
kuona mambo makubwa yanayofanywa na kamati kutokana na elimu 
mnayowapatia,mnastahili pongezi kubwa”alisema Bi.Kinyange.
“Mfano mzuri mimi ARUSHA nilipokua 
nafanya kazi, kamati zipo lakini kwakweli wamelala,unakuta kamati 
inakutana mara mbili kwa mwaka mzima,lakini huku ni zaidi ya mara 
kumi,kwakweli nimeshangaa sana,nyinyi ni shirika ambalo linafaa 
kuigwa,lakini wanakamati niwaombee mzidishe juhudi msiwaangushe 
wanauzikwasa na sisi kama halmashauri tutajitahidi kushirikiana kwa 
karibu kabisha na UZIKWASA ili kuendeleza juhudi hizi.”
Katika hatua nyingine mgeni huyo 
rasmi amempongeza kijana aliyeibuka mshindi katika shindano la kijana 
bora mfano wa kuigwa na kumtaka kuendeleza juhudi zake na kwamba 
Halmashauri watamtumia kama darasa kwa ajili ya vijana wengine kujifunza
 kutoka kwake.
Kwa upande wao kamati iliyoibuka 
mshindi kwa mwaka wa tatu mfululizo kutoka katika kijiji cha Mseko 
wamesema umoja na mshikamano ndio nguzo pekee ya ushindi wao,na kwamba 
shukrani pekee zinapaswa kwenda kwa UZIKWASA kwa mafunzo na ufuatiliaji 
wao kwani ndio vilivyowafanya kutekeleza mipango waliojiwekea kama 
wanakamati hadi kuibuka washindi.
‘Naweza kusema kamati yetu imejitoa 
sana,wanakamati wanatumia muda wao mwingi wa ziada katika kuhakikisha 
tunatekeleza mipango tuliojiwekea,lakini pia msukumo mkubwa ni kutoka 
UZIKWASA kwakweli tunawashukuru sana”Alisema Afisa mtendaji mseko.
Kwa upande wake Mratibu wa shughuli 
hizo kutoka shirika la UZIKWASA ambaye pia ni Afisa wa mradi wa jinsia 
na uongozi wenye mabadiliko, Bi.Salvata Kalanga amesema haikuwa kazi 
rahisi kuzipata kamati bora 8,kutokana na ushindani mkubwa uliokuwepo 
kwa washiriki 15,lakini wanashukuru kumpata mshindi ambaye wanaamini 
anastahili kutokana na kazi waliyoifanya.
Katika sherehe hizo,mshindi wa 
kwanza amepata zawadi ya ngao,pamoja na fedha taslimu shilingi laki 
sita,mshindi wa pili alipata laki 4 na nusu,na mshindi wa tatu alipata 
shilingi laki 4.
Sherehe ya kuzizawadia kamati bora 
za kudhibiti UKIMWI hufanyika kila mwaka chini ya shirika la 
UZIKWASA,lengo ni kuzipa motisha kamati hizo ili zifanye vizuri zaidi.
Mashindano haya na tamasha hili 
husimamiwa na kuwezeshwa na Asasi ya UZIKWASA Pangani kwa lengo na 
Kuamsha hamasa, kuchochea, kutafakari na kujifunza na kujenga 
uwajibikaji miongoni mwa vijana, akinamama na Kamati za Kudhibiti UKIMWI
 jinsia na uongozi za vijiji.
Mashindano haya huanza baada ya 
UZIKWASA kuwezesha kamati hizi kwa kuzijengea uwezo na baadae  maafisa 
wa  UZIKWASA kuzitembelea kamati hizo  na makundi yaliyotajwa na kupima 
utekelezaji wake kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa na kukubaliwa na 
wadau hao.
Kamati, vijana, na akina mama 
walioanishwa kufanya vizuri hutembelewa na kamati nyingine kuweza 
kujifunza kwa pamoja na kujirudhisha kwa utekelezaji wa kamati hizo. Pia
 kwa vijana na wakinamama hutembeleana na kupeana taarifa za utekelezaji
 na kujifunza kwa pamoja. Kamatai hizo na hao vijana na akinamama 
huchujwa na kubaki wachache ambao wanatekeleza vizuri zaidi.
Baada ya zoezi hilo la kutembeleana 
walioanishwa huitwa Pangani na kukutanishwa na waamuzi ambao 
huwasikiliza na kuchambua washindi.
Mwaka 2015 kamati 12 zilichaguliwa 
kuingia kwenye ushindani huo ambazo ni Mseko, Mwembeni, mkwajuni, 
mbulizaga, Bweni, mzambarauni, Mtonga, Mikocheni, Langoni,Tungamaa,  
Sange na Jaira.
Akina mama bora waliongia sita bora 
kati ya 33 ni kutoka Masaika, Kwa kibuyu, Stahabu, Mwembeni, Mtonga na 
Langoni. (watatu watazawadiwa)
Vijana bora waliongia sita bora kati ya 33 ni kutoka Msaraza, Kimanga, Mikocheni, Mseko, Boza na Mivumoni.(watatu watazawadiwa).
Mashindano haya yalianzishwa mwaka 
2010 ili kuleta msukumo, ushindani na chachu ya utekelezaji wa mipango 
ya vijiji ya ukimwi na maendeleo ya kijiji kwa ujumla na kuotesha mbegu 
ya uwajibikaji.
Mwaka 2010 Kamati ya Sanga iliibuka 
mshindi, mwaka 2011 kamati ya Langoni, iliibuka mshindi, mwaka 2012 
kamati ya Langoni iliibuka mshindi tena. Mwaka 2013 kamati ya Mseko 
iliibuka mshindi na mwaka 2014 Mseko iliibuka mshindi tena.
Mwaka huu wa 2015 mchuano ulikuwa 
mkubwa na kamati zimejituma na kuwajibika katika utekelezaji wa mipango 
yao ya maendeleo pamoja na kuyasaidia makundi mbalimbali yenye uhitaji.
Kamati kumi 15 zimetekeleza vizuri. 
Kamati  12 zimetekeleza wastani. kamati  6 ikiwepo, Ushongo, Kipumbwi, 
Masaika, Kigurusimba, kimang,a na Mivumoni  zinahitaji msukumo wa ziada 
kwa Kukosa uwajibikaji.
Mashindano haya yameleta msukumo 
katika  shughuli zote za kiuongozi na maendeleo ya vijiji. Palipo na 
uongozi mzuri na utekelezaji mzuri unakuwepo pia.
UZIKWASA itaendelea kuwajengea uwezo
 viongozi  wangazi zote na wanajamii kuweza kujitathmini, kuzama na 
kujichunguza  na kuweza kufanyia kazi changamoto za kiuongoza na 
kuwezesha maendeleo katika jamii. Suala la kupinga  unyanyasaji wa 
wanawake na watoto wa kike litapewa kipaumbele.
Kaimu mgeni rasmi ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii Bi.Patricia akizungumza na wananchi waliohudhuria katika tamasha hilo.
Burudani ya ngoma ilikua sehemu ya tamasha hilo.
Washehereshaji wa tamasha hilio, Pili Mlindwa na Shabani Kizamba wakiwajibika.
Wanakamati wa kijiji cha Mseko 
katika picha ya pamoja baada ya kutangazwa washindi, na wameibuka 
washindi kwa mwaka wa 3 mfululizo.
Mmoja wa wanakamati ya VMACK ya  kijiji cha mseko akicheza kwa furaha mbele ya meza kuu baada ya kutangazwa washindi,
Kaimu Mgeni rasmi Bi.Patricia akiwa ameshika ngao ambayo ni zawadi ya washindi wa VMACK kwa mwaka 2015.
Katibu wa kamati hiyo akipokea zawadi, Ngao na Hundi ya shilingi laki sita.
Vijana bora wa mfano wa kuigwa 
walioingia katika hatua ya 3 bora, na aliyeibuka mshindi ni kijana 
aliyevaa tshirt rangi ya njano.
Wamama walioingia katika tatu 
bora mama mfano wa kuigwa, na aliyeibuka mshindi ni mama ambaye 
ameshikilia pochi, ambaye anajulikana kwa jina maaarufu kuti kavu.
Hapa akipokea zawadi ya hundi ya shilingi laki 1 kwa kua mama/mwanamke bora mfano wa kuigwa kwa mwaka 2015.
Mwenyekiti wa kijiji cha Jaira 
akigawa zawadi ya sare za shule kwa viongozi wa vijiji vyote vya Wilaya 
ya PANGANI kwa niaba ya Aliyekua kijana bora mfano wa kuigwa mwaka 
2013-2014,ambayo aliahidi kwa watoto yatima alipochaguliwa.
Wamama wakifurahia jambo.
Sehemu/baadhi ya wananchi 
waliohudhuria katika tamasha la kuzizawadia kamati bora za kudhibiti 
UKIMWI, kijana bora na mama bora wa mfano wa kuigwa kwa mwaka 2015 
zilizofanyika katika kijiji cha JAIRA kata ya MADANGA Wilayani PANGANI.
Waandishi wa habari kutoka redio 
PANGANI FM, iliyochini ya shirika la UZIKWASA wakifuatilia kwa makini 
tamasha hilo (waliovaa tshirt za PANGANI FM).
Wananchi wa Pangani waliofika katika kijiji cha Jaira wakifuatilia kwa ukaribu tamasha hilo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni