FUNDI WA NDEGE AVUTWA NDANI YA INJINI YA NDEGE NA KUFA NCHINI INDIA

Fundi wa ndege wa shirika la ndege la Air India amekufa baada ya kuvutwa ndani ya injini ya ndege katika uwanja wa Mumbai.

Ajali hiyo imetokea wakati ndege aina ya AI 619 kutoka Mumbai kwenda Hyderabad ikirudi nyuma kujiandaa kuondoka, kwa mujibu wa shirika la Air India.

Mwenyekiti wa shirika la Air India Ashwani Lohani ameeieleza ajali hiyo kuwa ni ya bahati mbaya, lakini haijajulikana wazi nini kilitokea.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni