Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto) akisalimiana na 
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu wakati alipokuwa 
anawasili Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam kwa ziara ya 
kikazi. Waziri Kitwanga alifanya mazungumzo na Viongozi Wakuu wa jeshi 
hilo na kukubaliana kuweka mikakati zaidi ya kukabiliana na uhalifu 
nchini. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
Mkuu
 wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu akitoa taarifa mbalimbali 
za shughuli zinazofanywa na jeshi hilo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya 
Nchi, Charles Kitwanga (katikati), wakati Waziri huyo alipofanya ziara 
Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuzungumza 
na Viongozi Wakuu wa jeshi hilo, ambapo walikubaliana kuweka mikakati 
zaidi ya kukabiliana na uhalifu nchini.
Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akizungumza na waandishi wa
 habari (hawapo pichani) mara baada ya kumaliza mazungumzo na Viongozi 
Wakuu wa Jeshi la Polisi nchini. Waziri Kitwanga aliwaambia waandishi wa
 habari kuwa, wamekubaliana na Viongozi Wakuu wa jeshi hilo kuweka 
mikakati zaidi ya kukabiliana na uhalifu nchini. Wapili kushoto meza kuu
 ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu. Wapili kulia meza 
kuu ni Naibu IGP, Abdulharam Kaniki. Kulia ni Kamishna wa Oparesheni na 
Mafunzo wa Jeshi hilo, Paul Chagonja. Kushoto meza kuu ni Kamishna wa 
Polisi Jamii nchini, Mussa Ali Mussa. Kushoto ni Kamanda wa Polisi wa 
Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Suleiman 
Kova.
Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati waliokaa), Mkuu 
wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu (watatu kulia waliokaa) 
wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Wakuu wa Jeshi la Polisi 
nchini mara baada ya kikao chao kilichofanya katika Ukumbi wa Mikutano 
wa Makao Makuu ya Jeshi hilo kumalizika. Waziri Kitwanga alifanya 
mazungumzo na Viongozi hao na kukubaliana kuweka mikakati ya kupambana 
na uhalifu.
Msafara
 wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga ukiwasili katika 
lango Kuu la Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dar es Salaam kwa 
ajili ya kufanya mazungumzo na Viongozi Wakuu wa Jeshi hilo. Picha zote 
na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni