Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia) akimsalimia 
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester  Ambokile wakati alipowasili 
Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya 
ziara ya kikazi. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak 
Abdulwakil, na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, John Mngodo. Katika ziara 
hiyo, Waziri Kitwanga aliitaka Idara hiyo ya Uhamiaji kuanz rasmi kwa 
operesheni ya kuwakamata Wahamiaji Haramu nchini.
Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (aliyevaa tai) akiwasalimia
 wananchi wanaosubiri kupata huduma ya Hati za Kusafiria katika Ofisi za
 Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam. Waziri 
Kitwanga alifanya ziara ya kikazi katika ofisi hizo kwa lengo la 
kujifunza kazi mbalimbali zinazofanywa na Uhamiaji. Katika hotuba yake, 
licha ya maelekezo mengine aliyoyatoa kwa viongozi wakuu, pia aliitaka 
Idara hiyo ya Uhamiaji kuanza rasmi kwa operesheni ya kuwakamata 
Wahamiaji Haramu nchini.
Afisa 
Uhamiaji anayeshughulika na uchapaji wa Hati za  Kusafiria,  Amir Hassan
 (kushoto), akitoa maelezo ya jinsi wanavyozichapisha Hati za Kusafiria,
 kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) 
ambaye alifanya ziara ya kikazi katika ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji,
 Kurasini, jijini Dar es Salaam. Kulia ni  Kamishna Jenerali wa 
Uhamiaji, Sylvester  Ambokile.
Kamishna
 Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester  Ambokile (kushoto) akiwa na Waziri wa 
Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, wakati Waziri huyo alipokuwa 
anafanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar 
es Salaam kwa lengo la kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na 
Uhamiaji.
Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) akiwaeleza jambo
 Watendaji Wakuu wa Idara ya Uhamiaji wakati alipofanya ziara ya kikazi 
Makao Makuu ya idara hiyo, Kurasini, jijini Dar es Salaam leo. Wapili 
kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak 
Abduwakil, na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, John Mngodo, 
na wapili kulia (waliokaa) ni Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester  
Ambokile na kulia ni Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha),  Piniel 
Mgonja. 
Kamishna
 Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester  Ambokile akimfafanulia jambo Waziri wa
 Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) wakati Waziri huyo 
alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar
 es Salaam leo. 
Waziri
 wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (wasita kulia), Katibu Mkuu
 wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil (watano kushoto), Naibu Katibu Mkuu, 
John Mngodo (wanne kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi 
Wakuu wa Idara ya Uhamiaji wakati Waziri huyo alipotembelea Makao Makuu 
ya Idara ya Uhamiaji, Kurasini, jijini Dar es Salaam.  Wasita kushoto ni
 Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Sylvester  Ambokile. Picha zote na 
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni