Bwana Bony Lukas akieleza jinsi anavyofanya uraghbishi hasa katika kuwasaidia vijana kujua haki zao na kujitambua.
Na Fredy Njeje wa Blogs za Mikoa. 
Ni 
suala ambalo lipo wazi kuhusu tofauti za kimaisha baina ya wakazi wa 
mijini na vijijini, ila changamoto nyingi zaidi zinaonekana kuwakabili 
zaidi wale wanaoishi vijijini. Huko wananchi wanakosa huduma ambazo 
kimsingi ni haki zao na hivyo kutokuwa na usawa baina yao na wale wa 
mijini.
Picha 
kubwa inayojionesha vijijini kwa upande wa wanawake ni hasi kwa kiasi 
Fulani ukilinganisha na ile ya wanaume. Usawa wa kijinsia na kielimu 
baina yao na wanaume ni mkubwa sana, kesi za unyanyasaji kwao ni nyingi 
zaidi. Pamoja na jihudi nyingi za kuwawezesha wanawake bado hawajapata 
nafasi ya kutoshwa kuweza kusikilizwa. Wanaume wameendelea kuwa watoa 
maamuzi na wanufaikaji wa kimfumo. 
Mmoja wa waraghbishi akiwa anaonesha ripoti ya wanafunzi watoro katika shule ya msingi ya Nyandekwa .
Takwimu
 zinaonesha kuwa hata idadi ya ufauru kwa wasichana kwa Shule za msingi 
imeongezeka ambapo mwaka 2013 wasichana waliofaulu ni 281,460 sawa na 
asilimia 50.20 ya wanafunzi 560,706 wakati wavulana waliofaulu ni 
279,246 sawa na asilimia 49.80. Kabla ya ya matokeo wasichana waliofanya
 mtihani walikuwa 456,082 sawa na asilimia 52.68 na wavulana 409,745 
sawa na asilimia 47.32. Mwaka 2014 jumla ya watahiniwa 808,085 wa shule 
za msingi Tanzania wasajiliwa kufanya mtihani huo wakiwemo wasichana 
429,624 sawa na asilimia 53.17 na wavulana 378,461 sawa na asilimia 
46.83. Jumla ya watahiniwa 451,392 kati ya 792,118 walifanya mtihani, 
wasichana waliofauru ni 226,483 ambao ni sawa na asilimia 53.59 na 
wavulana 224,909 sawa na asilimia 46.41. 
Mraghishi Mariam Stephano (katikati) akieleza jambo wakati wa kikao.
Katika
 nchi yetu ya Tanzania kuna makabila zaidi ya 100 na kila moja likiwa na
 mila na tamaduni zake. Ni vizuri ikaeleweka kwamba wazee wetu hawakuwa 
wakichangamana kimakabila hivyo ni watu wachache walikuwa wanahama toka 
sehemu moja kwenda nyingine. Aina hii ya maisha ilipelekea wengi wao 
kuoana wa kabila moja, tofauti ikiwa ni vijiji ama kata, ila wengi 
ilikuwa toka mkoa ama wilaya moja. 
Tofauti
 na sasa ambapo watu wanachanganyikana kutokana na shughuli za kiuchumi 
na kijamii. Hali hii ya kuchanganyikana baina ya makabila ndani ya mkoa 
ama wilaya ama kijiji kimoja imeleta tamaduni tofauti na zile ambazo 
zilikuwa zimezoeleka kiuchumi na kijamii.
Pamoja
 na mchanganyiko huo bado kumekuwa na changamoto nyingi sana 
zinazowakabili wakazi wa vijijini. Bado wanaishi kwenye lindi la 
umaskini na ukosefu mkubwa wa huduma za kijamii. Changamoto hizi 
zinasababisha baadhi yao kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha wanadai
 na kusimamia haki za msingi za kijamii; hawa wanaitwa waraghbishi.
Waraghbishi
 ni mtu mmoja mmoja ama kikundi cha watu ambao wamevutika kufanya 
uraghbishi aidha kwa kufundishwa ama kwa kuona matokeo ya matendo 
wanayofanywa na wanajamii wenzao. Hususani wale ambao wanachukua hatua 
katika kustawisha au kulinda haki za binadamu na kuwakumbusha wenzao 
majukumu yao kwa maslahi ya kijamii, kiuchumi ama kisiasa.
Matilda
 Peter(wa pili kushoto) aliyeanza Uraghbishi 2015 akieleza namna 
anavyofanya Uraghbishi kwa kuwapa elimu wasichana juu ya kujitambua, na 
kuepuka mimba za utotoni
Moja 
ya haki hizo ni zile za wanawake ambao kwa muda mrefu wameonekana kuwa 
nyuma zaidi. Hali hii imewaondelea kujiamini na kujiona wao ni wa daraja
 la pili na hivyo kutokuwa na sauti katika jamii zao. 
Mmoja wa waraghbishi hao ni Bw. Bony Lukas toka kijiji cha 
Nyandekwa wilayani Kahama katika mkoa wa Shinyanga. Mraghbishi huyu 
ameweza kuelimisha watu wa kijiji chake. 
Akielezea jinsi anavyoraghbisha vijana katika kijiji chao, Lukasi anasema: 
“Vijana ndio wenye nguvu za kuweza kuleta maendeleo na ndio wenye 
mchango mkubwa ndani ya jamii zetu. Kwa hiyo ni lazima wawe ni watu 
wenye kujitambua katika nyanja zote. Ili waweze kupata nafasi mbalimbali
 za kuweza kutoa mchango wa mawazo ili yaweze kufanyiwa kazi” 
Hali inatokana na ukweli kwamba vijana wamekuwa nyuma kwa muda 
mrefu bila. Uraghbishi kwao ni mrejesho wa nafasi finyu ambazo vijana wa
 vijijini wamekuwa hawapewi nafasi ya kuweza kuchangia pindi wawapo 
katika mikutano ya kimaendeleo ndani ya vijiji. Hii ilitoa nafasi ya 
mraghbishi kupokea mawazo kutoka kwa vijana wa kike na wakiume kwani 
vijiji vilivyo vingi hupuuza mchango wa mawazo ya mtoto wa kike na 
kumuona hana thamani. 
Kwa mantiki hiyo mraghbishi Lukasi aliweza kuwatia ujasiri kwa 
kutoogopa kwani watakavyo kuwa na roho ya uoga ndio itakayo wafanya 
wabaki nyuma kimaendeleo. Kuna msemo unasema “woga wako ndio umaskini 
wako”. Hivyo alihakikisha anawawezesha vijana kujiamini na kushirikiana 
vyema na uongozi wa kijiji. 
Elimu ya jinsia pia ni tatizo katika vijiji vingi vya hapa 
Tanzania ambapo mraghbishi Miriam Stephano yeye aliweza kutumia nafasi 
hiyo kwa kuweza kuwaelimisha vijana kuhusu elimu ya jinsia. Akilielezea 
hilo anasema: 
“Hapa kijijini kuna vijana wa rika tofauti tofauti. Wapo wale 
ambao ndio wanabalehe na wale waliovuka hiyo ngazi ya kubalehe. 
Mabadiliko hayo ya kimaumbile hupelekea vijana wengi kuanza kuwa na 
muelekeo usio sahihi. Sababu ikiwa ni mihemko inayo wakumba pindi wawapo
 katika shughuli za kila siku hasa kwa wale wanao soma.” 
Mraghbishi Bujika Adam Joseph kutoka kijiji cha Guduba akitoa 
mchango wake wa namna alivyofanya uraghbishi kwa kuwahimiza vijana 
kuhudhuria mikutano ya vijiji ili nao wapate kushiriki katika kutoa 
mawazo na michango yao mbalimbali ya mawazo.
Vijana hawa katika kijiji hicho wanapata changamoto mbalimbali 
zinazotokana na mabadiliko ya kimaumbile. Hili linapeklekea kupata mimba
 za utotoni pamoja na maambukizi ya virusi vha Ukimwi. Hivyo kupitia 
waraghbishi vijana hawa wamekuwa wakipewa elimu ili waweze kujikinga na 
kujiepusha na hari zinakokuwa zikiendelea kuleta mabadiliko katika miili
 yao. 
Changamoto hii ndio iliyomplekea mraghbishi huyu mwanamke toka 
kijiji cha Nyendekwa, wilayani Kahama Bi. Mariam Stephano kuraghbisha 
kundi hili, kama anavyofafanua yeye mwenyewe: 
“Nikiwa kama mwanakijiji mraghbishi huwa ninapita katika mashule 
mbalimbali. Huko naomba ruhusa kwa mwalimu mkuu na kuweza kuzungumza na 
wanafunzi wa kike jinsi gani wanaweza kushughulika na mabadiliko ya 
miili yao. Nawaelekeza nini wafanye pindi wanapofikia umri wa kubalehe. 
Hapo ntawafundisha usafi wa mwili na namna ya kukwepa vishawishi 
vitakvyowapelekea aidha kupata maambukizi ya virusi vya Ukumwi ama mimba
 za utotoni”
Elimu hii ya jinsia inawasaidia watoto katika kijiji cha 
Nyandekwa, kwani wengi wao huanza kujitambua na kuwa na akili ya 
kutafakari yale yaliyo mema na mabaya. Na pia inawasaidia hata upande wa
 serikali katika dhana ya kupunguza maambukizi ya Ukimwi na magonjwa ya 
zinaa. 
Kwa upande wa mraghbishi Wilbert Michael kutoka kijiji cha Kakebe 
wilayani Kahama yeye alifanya utafiti usio rasmi juu ya tabia za uongozi
 wa kijiji chao. Hapo aliweza kugundua mambo kadhaa yaliyokuwa 
yakifanywa na viongozi wa kijiji hicho pasipo kuwashirikisha na 
wananchi. Na walifanya hivyo kwa maslahi binafsi. 
Akielezea hali hiyo, Michael anasema:
“Kupitia uraghbishi nilionao niliweza kufuatilia mambo mbalimbali 
katika ofisi ya kijiji pamoja na ile ya kata. Lengo ikiwa ni kubaini 
tatizo lililokuwa linakabili kijiji. Kubwa likiwa ni viongozi kujali 
maslahi binafsi, hapakuwa na uwazi kwenye mikataba ya kimaendeleo ya 
kijiji,”
Swali la kujiuliza yeye mraghbishi alijuaje habari hizo, akijibu swali hilo ansema:
“Nililigundua kupitia mbao za matangazo ambapo walibandika tangazo
 la kuingia kwa mkataba na watu wanao sambaza vyandarua vijijini na wao 
kuchukua kama ni mradi wa kujipatia kipato. Kupitia mradi vijana 
walitakiwa kugawa vyandarua hivyo, na hivyo ilikuwa ndio iwe ajira yao.”
Badala yake Mwenyekiti na Afisa Mtendaji wa kijiji wao wakawa 
wanawachangisha vijana fedha kiasi cha shilingi elfu kumi (10,000) kwa 
kila mmoja. Lengo lao likiwa ni kuwasajili kwa kuwa wasambazaji wa 
vyandarua hivyo kinyume cha dhana nzima ya kuleta maendeleo kijini. 
Na ndipo mraghbishi Michaeli alitumia uraghbishi wake kwa kuweza 
kuwataarifu wananchi na ndipo wananchi walipoamua kumwajibisha 
mwenyekiti huyo. Walichoamua ni kupeleka malalamiko katika ngazi 
mbalimbali za kata na wilaya ili waweze kumvua madaraka yake na 
kupendekeza jina la mweenyekiti mpya wanayemtaka na atakayeshirikiana na
 wanakijiji.
Hii ni dhahiri kwamba bado wananchi wanaoishi vijijini wanahitaji 
elimu ya kiraia itakayowawezesha kuwasilisha matatizo yao kwenye ngazi 
husika. Ili nao waweze kuwasaidia wenzao wanapogundua yale yanayofanywa 
na viongozi wao hayaendani na dhana ya ukweli na uwazi. Na piakuwa na 
ujasiri wa kuweza kuongea sehemu mbalimbali. 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni