SAMUEL ETO'O AMETEULIWA KUWA KOCHA WAMUDA WA TIMU YA ANTALYASPOR

Kapteni wa zamani wa Cameroon, Samuel Eto'o ameteuliwa kuwa kocha mchezaji wa muda wa timu ya Uturuki ya Antalyaspor.

Mshambuliaji huyo alijiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka mitatu inayoishia Juni mwakani, amepewa michezo mitatu ya majaribio ili kuuridhisha uongozi.

Eto'o amechukua wadhifa huo kutoka kwa Yusuf Simsek, ambaye mkataba wake ulikatizwa kwa makubaliano na uongozi wa timu hiyo Desemba 7.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni