Waziri
 wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango akitoa hotuba katika 
mkutano wa uzinduzi wa kitabu cha Mwongozo wa Usimamizi na Utayarishaji 
wa Miradi ya Uwekezaji katika sekta ya Umma kilichofanyika mjini Dodoma.
Waziri
 wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango akikata utepe kuashiria 
uzinduzi wa kitabu cha Mwongozo wa Usimamizi na Utayarishaji wa Miradi 
ya Uwekezaji katika sekta ya Umma, kushoto ni Katibu tawala wa mkoa wa 
Dodoma bibi. Rehema Madenge na kulia ni bi Anna Kimwela kutoka Tume ya 
Mipango.
Waziri
 wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango akionesha kitabu cha 
Mwongozo wa Usimamizi na Utayarishaji wa Miradi ya Uwekezaji katika 
sekta ya Umma (Public Investment Management Operational Manual), kulia 
ni Kaimu katibu mtendaji wa Tume ya Mipango Bibi Florence Mwanri na 
kushoto ni katibu tawala wa Mkoa wa Dodoma Bibi Rehema Madenge.
Waziri
 wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (wa tano kutoka kushoto kwa
 waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa mkutano mara baada
 ya uzinduzi wa kitabu cha Mwongozo wa Usimamizi na Utayarishaji wa 
Miradi ya Uwekezaji katika sekta ya Umma. 
 
                                                                                                  Na Adili Mhina, Dodoma 
Tume
 ya mipango imezindua kitabu cha Mwongozo wa Usimamizi na Utayarishaji 
wa Miradi ya Uwekezaji katika sekta ya Umma (Public Investment 
Management Operational Manual) kwa lengo la kuimarisha utendaji, 
uwajibikaji na kuleta ufanisi katika matumizi ya rasilimali za umma 
zinazoelekezwa katika miradi ya maendeleo. 
Akizindua mwongozo 
huo katika mkutano uliofanyika mwishoni mwa juma mjini Dodoma na 
kuhudhuriwa na wataalamu wa uchumi, sera na mipango kutoka wizara, 
halmashauri na taasisi mbalimbali za serikali,   Waziri wa fedha na 
mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango alieleza kuwa shabaha ya mwongozo huo ni
 kutoa maelekezo ya mchakato na hatua zinazohitajika kufuatwa katika 
kutayarisha na kutekeleza miradi yote inayotumia fedha za umma au kwa 
kushirikiana na sekta binafsi. 
Waziri mpango aliwataka viongozi 
wote wenye dhamana ya kusimamia miradi kusoma mwongozo huo na kuuelewa 
ili kuepuka makosa yaliyokuwa yakijitokeza huko nyuma huku akisisitiza 
kuwa serikali ya awamu ya tano haitamvumilia wala kumonea huruma 
mtendaji yeyote atakayeshindwa kuwajibika ipasavyo. 
“Kuanzia 
sasa watu ambao wamepewa dhamana ya kusimamia miradi ya maendeleo, 
miradi itakaposhindwa kuna mambo mawili tu yakufanya; ama waachie ngazi 
mapema wao wenyewe au basi wasubiri tuwatumbue. Kwahiyo nawaombeni sana 
hiki kitabu ambacho kimeandaliwa kuanzia leo kila mmoja akisome vizuri 
ili kusiwe na miradi tena ambayo ni ya ovyo ovyo,” alisisitiza waziri 
mpango. 
Mwongozo huo unazielekeza Wizara, Idarana 
Wakala wa Serikali,Sekretarieti za Mikoa na Serikali za Mitaa jinsi ya 
kufanya uchambuzi unaozingatia vigezo vya kiuchumi na kifedha na 
kufafanua mbinu, hatua, taratibu, na kuweka viwango vinavyohitajika 
katika kuandaa na kuwekeza miradi. 
Waziri Mpango alieleza kuwa 
maelekezo ya mwongozo huo yanafafanua vigezo muhimu vya uchambuzi wa 
kiuchumi na kifedha ili kufikia uamuzi wa miradi ipi ina manufaa na 
inaweza kupata mikopo katika soko la mitaji la ndani au la kimataifa. 
“Mwongozo
 huu umeanisha vigezo kama mzunguko wa mradi (project cycle) ikiwa ni 
pamoja na andiko la awali (concept note), mchanganuo wa faida na hasara 
(cost-benefit analysis) vigezo vya kuchanganua mradi kama vile uwezo wa 
uzalishaji (internal rate of return)  na thamani halisi ya uwekezaji 
(Net Present Value), na vinginevyo”Alieleza Dr. Mpango. 
Kuzinduliwa
 kwa mwongozo huo kunatoa tafsiri kuwa miradi yote itakayohitaji fedha 
za Serikali katika Bajeti italazimu kufuata utaratibu uliobainishwa 
katika kitabu hicho ili kuweza kuimarisha ufanisi na kupata thamani ya 
fedha. Hivyo, Mwongozo ni chombo muhimu katika michakato mbalimbali ya 
kupanga bajeti kama vile Mwongozo wa Mpango na Bajeti, Mpango wa 
Maendeleo wa Taifa wa Mwaka Mmoja na kadhalika. 
                                                                                                                               
Kwa
 upande wake Kaimu katibu mtendaji wa Tume ya Mipango Bibi Florence 
Mwandri alieleza kuwa mwongozo huo unategemewa kuwa mwanzo wa kujenga 
uwezo katika usimamizi wa uwekezaji wa umma na utakuwa ni msingi wa 
kuwaimarisha maafisa wa serikali kinyenzo katika kuchambua, kuchagua, 
kuwasilisha miradi ya uwekezaji kiuchumi na kifedha, pia kijamii kwa 
kukidhi taratibu na sheria zinazoendesha uwekezaji katika sekta ya umma.
 
“Katika kufanikisha utekelezaji wa Mwongozo huu na kujenga 
uwezo wa kutosha, Serikali imedhamiria kuweka utaratibu wa kutoa mafunzo
 kwa walengwa wakuu katika ngazi za mafunzo ya muda mfupi, muda wa kati 
na mrefu ili kuongeza utaalam na kuwekeza miradi michache kwa mwaka wa 
bajeti lakini kwa ufanisi zaidi”, alisema bibi Mwanri. 
Mwongozo 
huo pia unatoa taratibu kwa miradi ambayo haitapata fedha kwa mwaka 
husika itawekwa katika kanzi-data (Database) ambayo itaanzishwa chini ya
 Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango kwa ajili ya kufikia malengo ya 
utekelezaji wa usimamizi wa uwekezaji katika sekta ya umma. 
Kukamilika
 kwa kanzi-data kutasaidia wadau mbalimbali wanaohusika na maamuzi ya 
uwekezaji katika sekta ya umma kuwa na uelewa mmoja kuhusu miradi yenye 
kipaumbele. Kanzi-data itaonesha miradi gani ya umma, inategemewa 
kutekelezwa, itaanza lini, na kumalizika lini na ina fedha kiasi gani.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni