Na Rabi Hume, Modewjiblog, Mara
Kwa
 kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto, Taasisi ya Graca Machel kwa 
kushirikiana na serikali imefanya uzinduzi wa mradi ulio na malengo ya 
kuwarudisha shule watoto 20,000 waishio mkoa wa Mara ambao hawakupata 
nafasi ya kuwa shuleni.
Akizungumzia
 mradi huo, Mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Graca Machel alisema
 taasisi yake imeanzisha mradi huo kwa kutambua kuwa kuna idadi kubwa ya
 watoto walio nje ya shule kwa sababu mbalimbali hivyo kupitia mradi huo
 ni matarajio yao kuona watoto wakirudi shule ili kupata elimu ambayo 
itawasaidia kwa maisha yao ya baadae.
Aliongeza
 kuwa anatambua kazi aliyoifanya Mwalimu Nyerere kwa kuacha msingi bora 
wa elimu kwa watu wa aina zote na kuwataka wasimamizi wa mradi huo 
kuhakikisha wanafanikisha mradi kwa kuweka usawa baina ya watoto wa kike
 na watoto wa kiume ili wote wapate nafasi ya kurudi shule.
“Watoto
 wanatakiwa wawepo shuleni na wapate elimu bora bila kufanya upendeleo 
kwa watoto wa kike na watoto wa kiume ili wamalize pamoja elimu ya shule
 ya msingi na kuendelea na masomo wote wafikie malengo yao,
“Tunataka
 watoto wasio chini ya 20,000 warudi shule natambua Mwalimu (Nyerere) 
aliweka msingi bora wa elimu na ni haki ya watoto wote kupata elimu,” 
alisema Bi. Machel.
Mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Graca Machel akizungumza jambo kuhusu mradi huo. (Picha zote na Rabi Hume wa Modewjiblog )
Nae
 Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo aliishukuru Taasisi ya Graca 
Machel kwa kupeleka mradi huo mkoa wa Mara na kuahidi kuwa atakuwa 
kiongozi kufanikisha mradi huo ambao utafanyika kwa kipindi cha miaka 
miwili.
Pia
 alitumia fursa hiyo kutoa maagizo kwa watumishi walio chini yake 
kufanya kazi kwa juhudi katika maeneo yao pindi wanapohitajika kusaidia 
ili kufanikisha mradi huo ambao una malengo ya kuwasaidia watoto wa mkoa
 wa Mara kurudi shuleni.
“Nina
 shukuru sana kwa kuletewa mradi huu na Taasisi ya Graca Machel na 
nitashiriki kwa asilimia 100 kufanikisha mradi, na nitoe rai kwa 
watumishi wenzangu kuwa wafanye kazi kwa bidii kuanzia sasa tufanikishe 
mradi kama umevyopangwa,” alisema Mulongo.
Mkuu
 wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo akimshukuru mwanzilishi wa Taasisi ya 
Graca Machel, Graca Machel kwa kupeleka mradi huo mkoani kwake.
Aidha
 pamoja na kuzinduliwa kwa mradi huo, pia kunataraji kufanyika utafiti 
kutazama ni changamoto gani ambazo zilikuwa zinasababisha watoto wa mkoa
 huo kuwa nje ya shule, utafiti ambao utafanywa na Taasisi Huru ya 
Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF).
Akizungumzia
 utafiti huo, Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dkt. Tausi Kida alisema 
wanataraji kuanza kufanya utafiti kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza
 itafanyika mwezi huu Aprili na awamu ya pili itafanyika mwezi Julai.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida akizungumzia utafiti unatarajiwa 
kufanywa na ESRF kuhusu changamoto ambazo zilikuwa zinasababisha watoto 
wa mkoa wa Mara kuwa nje ya shule wakati wa uzinduzi wa mradi ulio na 
malengo ya kuwarudisha shuleni watoto 20,000.
“Utafiti
 huu ambao unamalengo ya kufanikisha watoto 20,000 wa mkoa wa Mara 
kurudi shuleni utafanyika kwa awamu mbili, unaanza Aprili kwa maeneo ya 
Musoma, Bunda, Rorya, Butiama na Wilaya ya Tarime,
“Awamu
 ya pili itafanyika kuanzia mwezi Julai kwa eneo la Manispaa ya Musoma, 
Bunda Mjini, Tarime Mjini, Serengeti na Magumu,” alisema Dkt. Kida.
Mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Graca Machel akiweka saini ya kuashiria kufanyika kwa mradi huo.
Watiliaji saini ya makubaliano ya mradi huo wakiwa katika picha ya pamoja.
Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dkt. Tausi Kida akizungumza jambo na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo.
Mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Graca Machel akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dkt. Tausi Kida.
Baadhi
 ya washiriki katika uzinduzi wa mradi huo, Wa kwanza Kushoto ni 
Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dkt. Tausi Kida, Mwanzilishi wa Taasisi ya 
Graca Machel, Graca Machel, Askofu Michael Msongazira wa Kanisa la 
Roman, Musoma na Mkuu wa Idara ya Utafiti na Machapisho wa ESRF, Prof. 
Fortunata Makene.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni