Katibu
 Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John William Kijazi akifungua mafunzo ya 
Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma yalioandaliwa na Ofisi ya Rais, 
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma leo jijini Dar es salaam. 
Kushoto ni Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji 
Mstaafu Salome Kaganda.
Kamishna
 wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Salome 
Kaganda akitoa maelezo mafupi yanayohusu Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya 
Maadili ya Viongozi wa Umma wakati wa mafunzo ya Wakuu wa Mashirika na 
Taasisi za Umma leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi 
Balozi Mhandisi John William Kijazi.
Baadhi
 ya Washiriki wa mafunzo ya Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma 
waliohudhuria mafunzo ya maadili yaliyoandaliwa na Ofisi ya Rais, 
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma leo jijini Dar es salaam.
Baadhi
 ya Washiriki wa mafunzo ya Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma 
waliohudhuria mafunzo ya maadili yaliyoandaliwa na Ofisi ya Rais, 
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu 
Kiongozi Balozi Mhandisi John William Kijazi (hayupo pichani) leo jijini
 Dar es salaam.
Baadhi
 ya Washiriki wa mafunzo ya Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma 
waliohudhuria mafunzo ya maadili yaliyoandaliwa na Ofisi ya Rais, 
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu 
Kiongozi Balozi Mhandisi John William Kijazi leo jijini Dar es salaam.
Katibu
 Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John William Kijazi akiongea na Waandishi
 wa habari mara baada ya kufungua mafunzo ya Wakuu wa Mashirika na 
Taasisi za Umma yalioandaliwa na Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili 
ya Viongozi wa Umma leo jijini Dar es salaam.(Picha na Eleuteri 
Mangi-MAELEZO).
Katibu
 Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John William Kijazi amewaasa Wakuu wa 
Mashirika na Taasisi za Umma kuzingatia Maadili ya Viongozi wa Umma 
katika kutekeleza makujumu yao.
Katibu
 Mkuu alisema hayo leo jijini Dar es salaam wakati wa akifungua mafunzo 
ya viongozi hao yalioandaliwa na Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Maadili 
ya Viongozi wa Umma ili kuhakikisha wanaendana Uongozi wa Serikali ya 
Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Mgufuli.
“Maadili
 yana umuhimu wake mkubwa katika utawala wa maendeleo ya nchi, kupitia 
maadili mema wananchi wanajenga imani na viongozi pamoja na Serikali yao
 kwa ujumla” alisema  Balozi Mhandisi Kijazi.
Ili
 kuhakikisha mafunzo yanakuwa yenye tija, Balozi Mhandisi Kijazi 
amewasisitiza viongozi hao kutumia muda vizuri na kujikumbusha na 
kujifunza maadili hayo kwa manufaa ya mashirika na taasisi zao pamoja na
 taifa kwa ujumla.
Balozi
 Mhandisi Kijazi alitaja umuhimu wa maadili katika jamii na kusema kuwa 
yanasaidia kusimamia rasilimali za umma na kuzitumia kwa maslahi ya 
wote, kuongeza tija na thamani ya huduma, zinazotolewa na Serikali, 
kudhibiti mianya ya ukiukwaji wa  maadili na vitendo vya rushwa, kujenga
 ujasiri wa kusimamia Sheria, Kanuni na Taratibu za utumishi wa umma.
Maadili
 pia yanasaidia wananchi, viongozi na Watumishi wa Umma kutoa mchango wa
 haraka katika kutekeleza maendeleo ya nchi, kuepuka utata wa maamuzi ya
 migongano ya kimaslahi, kuwavutia wawekezaji, kujenga na kudumisha 
amani na utulivu pamoja na kuondoa na kukomesha ubinafsi kwa viongozi.
Aidha,
 Katibu Mkuu Kiongozi Balozi  Kijazi amesema kuwa ukiukwaji wa maadili 
unaathari hasi kwa taifa ambapo alizitaja baadhi ya athari hizo kuwa ni 
rasilimali za nchi kunufaisha wachache, wananchi kukosa haki zao za 
msingi kutokana na rushwa na upendeleo, viongozi wa umma kujilimbikizia 
mali isivyostahili bila kujali hali za wananchi wanaowaongoza, kupungua 
kasi ya uwekezaji pamoja na kudhohofika kwa uchumi wa nchi.
Madhara
 mengine ya kutojali maadili ni wananchi kukosa imani na Serikali yao, 
kuchochea vurugu pamoja na wananchi kutotii sheria za nchi na hivyo 
kuhatarisha usalama, amani na utulivu wa nchi.
Kwa
 upande wake Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma 
Jaji Mstaafu Salome Kaganda alipokuwa maelezo mafupi kwa Mgeni Rasmi 
amesema kuwa misingi ya maadili na maadili yanalenga katika kuzuia 
mgongano wa maslahi, upendeleo, matumizi mabaya ya rasilimali za umma na
 taarifa za ofisi na mwenendo usiofaa kwa viongozi wa umma ili 
kuimarisha na kuendeleza dhana za uadilifu, uwajibikaji na uwazi  ambazo
 ni sifa muhimu za kiongozi.
Ili
 kuongeza ufanisi katika utendaji kazi, Jaji Mstaafu Kaganda amesema 
kuwa ofisi yake inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa
 watumishi ambapo kuna zaidi ya viongozi 15,000 huku Sekretarieti ina 
wafanyakazi 200 nchi nzima.
 Mafunzo
 hayo yamehudhuriwa na washiriki 40 ambapo yalifanyika kwa Mawaziri, 
Manaibu Waziri, Mkatibu Wakuu, Manaibu Katibu Wakuu, Wenza wa Viongozi, 
Wakuu wa Mikoa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni