WAZIRI PROF. MBARAWA AKAGUA DARAJA LA RUSUMO NA VITUO VYA PAMOJA VYA FORODHA KABLA YA UFUNGUZI.

LUS5
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (katikati) akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Sekta ya Ujenzi Eng. Joseph Nyamhanga (kushoto) na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Eng. Patrick Mfugale wakati akikagua Daraja la Rusumo wilayani Ngara.
LUS1
Muonekano wa barabara ya Nyakahura-Rusumo inayounganisha Tanzania na Rwanda kupitia Daraja la Rusumo wilayani Ngara.

LUS2
Mtaalam kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wa pili kulia akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa tatu kulia), alipotembelea ofisi hizo katika Kituo cha pamoja cha forodha (One Stop Border Post) upande wa Tanzania kilichopo Rusumo wilayani Ngara, wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Sekta ya Ujenzi Eng. Joseph Nyamhanga.
LUS3
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akitoa ufafanuzi kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Eng. Patrick Mfugale (mwenye kofia) wakati akikagua maandalizi ya ufunguzi wa Daraja la Rusumo na Vituo vya pamoja vya forodha (One Stop Border Post) wilayani Ngara.
LUS4
Muonekano wa Daraja la Rusumo linalounganisha Tanzania na Rwanda, kushoto ni daraja la zamani lenye rangi ya njano na kulia ni daraja jipya.
LUS6
Meneja wa Kituo cha pamoja cha forodha(One Stop Border Post), katika mpaka wa Tanzania na Rwanda upande wa Rwanda Bw. Moses Kalisa akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa na ujumbe wake walipotembelea kituo hicho.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni