Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Maji, Nishati Ardhi na Makaazi  Ali Khalil Mirza na 
Makamu wa Rais wa Kampuni ya Multiconsult ya Norway Oyvi’nd Holtedahl 
wakipongezana mara baada ya kusaini Mradi wa kuimarisha huduma za umeme 
Zanzibar. 
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Maji , Ardhi,  Nishati na Makaazi Ali Khalil Mirza, 
akitoa maelezo juu ya mradi wa kuimarisha huduma za Umeme Zanzibar, 
kabla ya kutiliana saini makubaliano ya miaka mitatu na nusu na Serikali
 ya Norway katika hafla iliyofanyika  Makao Makuu ya Wizara Forodhani 
Mjini Zanzibar.
Mshauri
 mwandamizi wa Kampuni ya Multiconsult ya Norway Andrew Yager akitoa 
shukurani kwa Serikali ya Zanzibar kwa kuichagua kampuni yao katika kazi
 za kuimarisha huduma ya umeme  katika hafla ya kutilina saini 
makubaliano ya mradi huo.
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya  Maji, Nishati  Ardhi na Makaazi  Ali Khalil Mirza 
(wa kwanza kulia waliokaa) na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Multiconsult 
ya Norway Oyvi’nd Holtedahl wakitia saini makubaliano ya kuimarisha 
huduma za umeme Zanzibar katika hafla iliyofanyika leo Makao Makuu ya 
Wizara, Forodhani Mjini Zanzibar. Picha na Makame Mshenga, Maelezo Zanzibar.
                                                                            Na Miza Othman-Melezo Zanzibar  
SERIKALI
 ya Mapinduzi Zanzibar,  imetiliana saini na Serikali ya Sweden 
makubaliano ya kuimarisha huduma za  nishati ya umeme hapa nchini. 
Katika
 hafla ya utiaji saini wa mradi huo, Zanzibar iliwakikishwa na Katibu 
Mkuu wa Wizara ya  Maji, Ardhi, Nishati na Makaazi  Ali Khalil Mirza, 
wakati Makamu wa  Rais Mtendaji wa Kampuni ya Multi Consult kutoka 
Norway Oyvind Holtedahl, alisaini kwa niaba ya Serikali ya Sweden. 
Katika
 hafla hiyo iliyofanyika Makao makuu ya Wizara ya Maji, Ardhi, Nishati 
na Makaazi  Katibu Mkuu Mirza, alisema kampuni ya Multi Cionsult 
ilishinda zabuni hiyo kati ya kampuni 12 zilizoomba kutekeleza mradi 
huo. 
Alieleza kuwa mradi huo utakaochukua miaka mitatu na nusu 
hadi kukamilika kwake, utagharimu shilingi bilioni 12.7 za Kitanzania. 
Amefahamisha
 kuwa, miongoni mwa matumizi ya fedha hizo, ni kuwapatia mafunzo 
wafanyakazi wa wizara hiyo ili kuwajengea uwezo wa kufanya tafiti ili 
wafanye kazi zao kwa ufanisi.     
Mirza alieleza kuwa, lengo la 
Kampuni hiyo ni kusaidia katika kulijengea uwezo Shirika la Umeme 
Zanzibar (ZECO) pamoja na Idara zake kuhusu sera ya nishati  ambayo ni 
muhimu kwa maenedeleo ya taifa. 
Naye Mshauri Mwandamizi  wa 
Kampuni ya Multi Consult ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar 
kwa kuwaamini kufanya kazi hiyo na ameahidi kuwa wataitekeleza kwa 
ufanisi mkubwa.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni