SMZ IMETILIANA SAINI NA NORWAY MAKUBALIANO YA KUIMARISHA SEKTA YA UMEME

sw1
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Nishati Ardhi na Makaazi Ali Khalil Mirza na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Multiconsult ya Norway Oyvi’nd Holtedahl wakipongezana mara baada ya kusaini Mradi wa kuimarisha huduma za umeme Zanzibar.
sw2
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji , Ardhi, Nishati na Makaazi Ali Khalil Mirza, akitoa maelezo juu ya mradi wa kuimarisha huduma za Umeme Zanzibar, kabla ya kutiliana saini makubaliano ya miaka mitatu na nusu na Serikali ya Norway katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Wizara Forodhani Mjini Zanzibar.
sw3
Mshauri mwandamizi wa Kampuni ya Multiconsult ya Norway Andrew Yager akitoa shukurani kwa Serikali ya Zanzibar kwa kuichagua kampuni yao katika kazi za kuimarisha huduma ya umeme katika hafla ya kutilina saini makubaliano ya mradi huo.
sw4
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Nishati Ardhi na Makaazi Ali Khalil Mirza (wa kwanza kulia waliokaa) na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Multiconsult ya Norway Oyvi’nd Holtedahl wakitia saini makubaliano ya kuimarisha huduma za umeme Zanzibar katika hafla iliyofanyika leo Makao Makuu ya Wizara, Forodhani Mjini Zanzibar. Picha na Makame Mshenga, Maelezo Zanzibar.


                                                                            Na Miza Othman-Melezo Zanzibar

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar, imetiliana saini na Serikali ya Sweden makubaliano ya kuimarisha huduma za nishati ya umeme hapa nchini.

Katika hafla ya utiaji saini wa mradi huo, Zanzibar iliwakikishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Ardhi, Nishati na Makaazi Ali Khalil Mirza, wakati Makamu wa Rais Mtendaji wa Kampuni ya Multi Consult kutoka Norway Oyvind Holtedahl, alisaini kwa niaba ya Serikali ya Sweden.

Katika hafla hiyo iliyofanyika Makao makuu ya Wizara ya Maji, Ardhi, Nishati na Makaazi Katibu Mkuu Mirza, alisema kampuni ya Multi Cionsult ilishinda zabuni hiyo kati ya kampuni 12 zilizoomba kutekeleza mradi huo.

Alieleza kuwa mradi huo utakaochukua miaka mitatu na nusu hadi kukamilika kwake, utagharimu shilingi bilioni 12.7 za Kitanzania.

Amefahamisha kuwa, miongoni mwa matumizi ya fedha hizo, ni kuwapatia mafunzo wafanyakazi wa wizara hiyo ili kuwajengea uwezo wa kufanya tafiti ili wafanye kazi zao kwa ufanisi.

Mirza alieleza kuwa, lengo la Kampuni hiyo ni kusaidia katika kulijengea uwezo Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) pamoja na Idara zake kuhusu sera ya nishati ambayo ni muhimu kwa maenedeleo ya taifa.

Naye Mshauri Mwandamizi wa Kampuni ya Multi Consult ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwaamini kufanya kazi hiyo na ameahidi kuwa wataitekeleza kwa ufanisi mkubwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni