Baadhi
 ya Nyumba za makazi, huduma mbalimbali na vijiwe vya kufanyia biashara 
eneo la Chalinze nyama Dodoma vikiwa vimezingirwa na maji (mafuriko) 
kufuatia mvua kubwa iliyonyesha mkoani humo usiku wa kuamkia April 4, 
2016.
Baadhi
 ya Wakazi wa eneo la Chalinze nyama Dodoma wakihamisha mali zao baada 
ya makazi yao kuzingirwa na maji (mafuriko) kufuatia mvua kubwa 
iliyonyesha mkoani humo usiku wa kuamkia April 4, 2016.
Baadhi
 ya magari  ya kubeba abiria mapema  yalinusurika kusombwa na 
mafuriko yalipojaribu kuvuka barabara eneo la Chalinze nyama Dodoma 
kufuatia mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha usiku wa 
kuamkia April 4, 2016.
Safari
 za magari ya abiria na mizigo zilikwama eneo la Chalinze nyama Dodoma 
kwenye barabara itokayo Dodoma kuelekea Dar es salaam kuanzia alfajiri 
ya Aprili 4, 2016 hadi alasiri kufuatia mafuriko yaliyosababishwa na 
mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia siku hiyo.
Mkuu
 wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Jordan Rugimbana akiwa na Mkuu wa Wilaya ya 
Chamwino Mhe. Farida Mgomi (katikati) na viongozi wengine wakikagua eneo
 la Barabara eneo la Chalinze nyama ili kuona namna ya kupitisha magari 
ya abiria na mizigo yaliyokwama tangu alfajiri ya Aprili 4, 2016 hadi 
alasiri kufuatia mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha 
usiku wa kuamkia siku hiyo.
Magari
 ya abiria na mizigo yanayokadiriwa kuwa zaidi ya 1,000 ambayo yalikwama
 eneo la Chalinze nyama Dodoma kwenye barabara itokayo Dodoma kuelekea 
Dar es salaam kuanzia leo alfajiri hadi alasiri kufuatia barabara hiyo 
kufungwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha usiku wa
 kuamkia  April 4, 2016.
Mkuu
 wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Jordan Rugimbana akishuhudia magari ya mizigo na
 abiria yakiendelea na safari  Alasiri baada ya kuruhusiwa kufuatia 
kupungua kwa maji (mafuriko) yaliyofunga barabara kuu ya Dodoma Dar es 
salaam eneo la Chalinze nyama Dodoma tangu alfajiri.
Mkuu
 wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Jordan Rugimbana (kushoto) akiijulia hali kaya 
iliyonusurika kusombwa na mafuriko kufuatia makazi yao kuzungukwa na 
maji mengi eneo la chalinze nyama yaliyosababishwa na mvua kubwa 
iliyonyesha usiku wa kuamkia  April 4, 2016.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni