MTOTO PRINCE GEORGE AWA STAA BAADA YA KUSALIMIANA NA RAIS OBAMA

Mtoto Prince George amekuwa nyota kwenye pati ya Kensington Palace baada ya kusalimiana na rais Barack Obama akiwa amevalia mavazi ya kulala pamoja na kandambili.

Pati hiyo ya mlo wa jioni ilikuwa inakamilisha ratiba ya ziara ya rasi Obama nchini Uingereza aliyopanga kukutana na viongozi wa ngazi za juu wa taifa hilo.

Prince George pia alikutana tena na rais Obama wakati alipokuwa anacheza na farasi wa kuchonga aliopewa awali na rais huyo kama zawadi.
  Rais Obama, Prince William na mkewe Kate wakimuangalia Prince George akicheza na farasi wakati wa pati hiyo iliyofanyika nyumbani kwa wanafamilia hiyo ya kifalme.
  Rais Obama akiongea na Prince William, pia alikuwemo Prince Harry, Michelle Obama na Kate
   Michelle Obama akiongea na Kate ambaye anaonekana akimsikiliza kwa umakini

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni