Kutokana
 na kukua kwa huduma za kibenki kupitia simu za mkononi (mobile 
banking), Watanzania wametakiwa kutumia nafasi hiyo vizuri ili iweze 
kuwasaidia kukuza uchumi wao.
Akizungumza
 na waandishi wa habari katika mkutano wa siku mbili unaozungumzia 
maendeleo ya sekta za fedha kwa kutumia mifumo ya huduma za kibenki kwa 
kutumia mitandao ya simu (Africa Digital Banking Summit), Naibu Waziri 
wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji amesema ni muda muafaka kwa 
Watanzania kutumia huduma hizo kwa ajili ya kujiongezea kipato.
Alisema
 kupitia huduma hizo, Watanzania wanaweza kutuma nakupokea pesa kutoka 
maeneo mbalimbali hata ambayo yapo mbali na matawi ya benki hivyo 
wanaweza kufanya shughuli mbalimbali ikiwepo kufanya biashara kwa 
kutumia huduma hizo.
“Serikali
 imeunganisha nchi nzima na mkongo wa taifa na hii inawapa fursa 
watanzania kutuma pesa sehemu yoyote hivyo niwasihi watanzania kutumia 
kikamilifu nafasi hiyo ili kuboresha uchumi wao,” amesema Dkt. Kijaji.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji akitoa hotuba katika mkutano huo. (Picha zote na Rabi Hume, Modewjiblog)
Nae
 Mkurugenzi Mkuu wa NMB nchini, Ineke Bussemaker amesema kuwepo kwa 
huduma za kibenki kupitia mitandao ya simu kumewezesha wateja wao kupata
 huduma kirahisi tofauti na miaka ya nyuma kabla ya kuanza kwa huduma ya
 mobile banking.
Alisema
 kupitia huduma hiyo kwa sasa wateja wao wanauwezo wa kutoa fedha, 
kulipia huduma mbalimbali kama kodi, kununua umeme, tiketi za ndege na 
hata kuangalia salio lililo katika akaunti zao za benki na 
wanachokifanya kwa sasa ni kuangalia jinsi gani wanaboresha zaidi huduma
 hizo kwa wateja hasa walio maeneo ya vijijini.
“Miaka
 ya nyuma kama mteja yupo kijijini anatumia muda mwingi kwenda sehemu 
iliyo na huduma ya benki lakini kwa sasa huduma za kibenki katika 
mitandao ya simu imerahisisha hata wateja wetu walio vijijini kupata 
huduma zetu kiurahisi,” amesema Bi. Bussemaker.
Nae
 Meneja wa Mifumo wa Malipo wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Bernard Dadi
 amesema huduma za kibenki kwa kutumia mitandao ya simu imekuwa ikizidi 
kukua siku baada ya siku tangu ilipoanza nchini mwaka 2008 na mpaka sasa
 kuna benki 30 ambazo zimejiunga katika mfumo huo ili kuwasogezea huduma
 wateja wake.
 Meneja Mifumo ya Malipo wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Bernard Dadi akitoa taarifa kuhusu matumizi ya mobile banking nchini.






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni