Mkuu
 wa Idara ya Maarifa na Ubunifu wa ESRF, Bi. Margareth 
Nzuki akiwasilisha malengo ya warsha kabla ya kumkaribisha Mkurugenzi 
Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi 
Kida kufungua warsha hiyo.
Wajasiriamali
 kutoka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam wamefanikiwa kupata 
nafasi ya mafunzo yanayohusu fursa mpya zinazopatikana katika kilimo cha
 biashara katika warsha iliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na
 Jamii (ESRF).
Elimu
 ambayo wajasiriamali waliipata katika warsha hiyo ni elimu ya shamba 
kitalu na ujasiriamali, elimu ya kilimo cha foda na mbogamboga, elimu ya
 kilimo na kufuga samaki katika matanki, elimu ya ufugaji samaki katika 
mabwawa, elimu ya ufugaji samaki katika vizimba, kutazama fursa zilizopo
 katika ufugaji bora wa kuku na kupata elimu kuhusu Azolla ambayo 
inaweza kutumika kama chakula cha mifugo na pia kama mbolea.
Akizungumza
 katika warsha hiyo mmoja wa wawasilishaji mada, Dominic Haule alisema 
kilimo kina fursa nyingi lakini watu wengi wanashindwa kufanikiwa 
kutokana na kuwepo mambo mbalimbali ambayo yanayakwamisha.
Alisema
 changamoto hizo ni pamoja na kukosa elimu ya kilimo na kushindwa kupata
 taarifa sahihi za kiteknolojia kuhusu kilimo cha kisasa.
“Tunahitaji
 kutazama fursa zilizopo, zipo nyingi lakini bado tunakabiliwa na 
changamoto wakulima wanakosa elimu ya kilimo kujua hata mazao bora 
yanakuwaje, bado kuna shida ya pembejeo na mitaji inakuwa changamoto 
maana ili ufanikiwe unahitaji uwekezaji mkubwa,” alisema Haule.
Awali
 akitoa neno la ufunguzi, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa 
Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida alisema Tanzania ina maeneo 
mazuri ya kufanyia kilimo na kinachohitajika ni wakulima kutambua njia 
za kufanya kilimo bora ili watakapoanza kulima waweze kupata matokeo 
mazuri kwa aina ya kilimo wanachofanya.
“Uchumi
 wa nchi unategemea kilimo, nchi yetu ina eneo zuri la kilimo lakini 
bado kuna changamoto kama mabadiliko ya hali ya nchi ni vyema kukutana 
na kujua njia bora za kutumia kabla ya kuanza kufanya kilimo,” alisema 
Dkt. Kida.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi
 Kida akifungua warsha ya siku moja yenye lengo la kutambulisha na 
kuelimisha zaidi wananchi kuhusu fursa mpya za kibiashara ambazo 
zinapatikana katika sekta ya Kilimo.
Mshereheshaji katika warsha ya kutazama fursa mpya katika kilimo biashara, Abdallah Hassan.
Mwakilishi
 wa Wizara ya Kilimo, Mifungo na Uvuvi , John Mapunda akielezea nafasi 
ya serikali kuwasaidia wajasiriamali ili kufikia malengo yao katika 
warsha ya siku moja iliyoandaliwa na ESRF.
Pichani
 juu na chini ni umati wa washiriki kutoka mikoani na maeneo mbalimbali 
ya jiji la Dar es Salaam waliohudhuria warsha hiyo iliyoandaliwa na 
ESRF.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi
 Kida akifurahi jambo na mwakilishi wa Wizara ya Kilimo, Mifungo na 
Uvuvi, John Mapunda katika warsha hiyo.
Dominic Haule kutoka chuo cha iMADS akielezea kuhusu shamba kitalu na ujasiriamali.
Bw.
 Abdullatif Mbulo kutoka Horti Ogranics Ltd, akielezea kuhusu kilimocha 
foda na mbogamboga, sambamba na ufugaji wa samaki katika matanki.
Luteni
 Joseph Lyakulwa, kutoka Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) akizungumzia 
Ufugaji wa Samaki katika Vizimba katika warsha hiyo iliyohudhuriwa na 
wajasiliamali mbalimbali.
Pichani
 juu na chini washiriki wakifuatilia kwa umakini mada mbalimbali 
zilizokuwa zikiwasilishwa na wataalamu wa Kilimo Biashara.
Pichani
 juu na chini washiriki wakiuliza maswali kwa wawasilishaji mada katika 
warsha ya siku moja ya Kilimo Biashara iliyoandaliwa na ESRF.
Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dkt. Tausi Kida akizungumza na waandishi wa habari.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni