Na Mwandishi Wetu, Dodoma 
MKUU
 wa mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana ameipongeza timu ya Uchukuzi SC kwa
 kuleta wachezaji wengi kwenye mashindano ya Mei Mosi yaliyoanza Aprili 
18 mwaka huu kwenye uwanja wa Jamhuri Dodoma. 
Mh. Rugimbana 
katika hotuba ya ufunguzi wa mashindano hayo iliyosomwa jana na Afisa 
Maendeleo Vijana wa ofisi ya mkuu wa mkoa, Tumsifu Mwasambale kwa niaba 
yake, alisema kuwa amedokezwa na waandaaji kuwa Uchukuzi SC ndio timu 
pekee iliyoweza kuleta wachezaji wengi, hivyo anawapongeza viongozi wao.
 
“Ninaipongeza Uchukuzi SC pamoja na kudokezwa pia nimeona kwa 
macho yangu wakati wa maandamano ya timu zikiingia uwanjani  kuwa 
Uchukuzi SC ndio wenye wachezaji wengi zaidi, nawapongeza sana viongozi 
wao, wanatambua umuhimu wa michezo mahala pa kazi,” alisema. 
Kwa
 mujibu wa Katibu Mkuu wa timu ya Uchukuzi SC, Alex Temba amesema timu 
yake imekuja na wachezaji takribani 96 ambao watashiriki kwenye michezo 
ya kuvuta kamba, netiboli, riadha, kuendesha baiskeli, soka, bao, karata
 na darts. 
Tayari timu hiyo inayoundwa na wachezaji kutoka 
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Bandari (TPA), Anga (TCAA), Hali ya 
Hewa (TMA) na Chuo cha Bandari (DMI),  imeshinda kwenye mechi zake za 
soka dhidi ya Ukaguzi magoli 3-1 na upande wa netiboli waliwafunga CDA 
magoli 23-15. 
Hatahivyo, Mh. Rugimbana aliwashutumu na kusema 
sababu zilizotolewa na viongozi hao kuzuia timu zao kushiriki kwenye 
mashindano ya mwaka huu kwa kisingizio cha Mh. Rais John Magufuli kuzuia
 michezo hii, hazina mashiko na ni kisingizio kilichopaswa kukemewa 
vikali. 
Alisema hajawahi  kumsikia Mh. Rais Magufuli akizuia 
michezo ya Mei Mosi, na mingine yeyote bali walimsikia akitoa maelekezo 
ya kuzuia sherehe za Uhuru na sasa Muungano, na kutoa maelekezo na 
tayari yanmefatwa kwa ufanisi mkubwa na wahusika. 
“Ni uoga 
usiokuwa na mashiko, kwani hata ingekuwa Mh Rais kazuia michezo,  hata 
Mh. Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa) asingekuwa na nguvy ya kukutana na 
viongozi wa mashirikisho na vyama vya michezo Uwanja wa Taifa, Dar es 
Salaam, takribani miezi mitatu iliyopita wakijadili uimarishaji wa 
michezo, na walaumu sana viongozi  waliowanyima haki wanamichezo 
kushiriki kwenye michezo hii,” alisema Rugimbana. 
Mashindano ya 
mwaka huu yenye kauli mbiu ya hapa kazi tu isiwe kisingizio kwa waajiri 
kuondoa michezo kazini, yamekuwa na idadi ndogo ya washiriki, ambapo 
hadi jana ni timu 14 pekee ndizo zilizofika Dodoma. 
Hatahivyo, 
awali Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mei Mosi, Joyce Benjamin, 
naye katika hotuba ya ufunguzi aliwalaumu viongozi kuzuia timu zao kwa 
kumsingizia Mh. Rais kuwa amezuia michezo. 
 “Kumbukeni Mh. Rais 
wetu ni mmoja wa wanamichezo na ndio maana hata wakati wa kampeni 
tulimuona wote akipiga pushapu jukwaani, sasa iweje leo hii viongozi wa 
sehemu za kazi waseme amekataza michezo, michezo huu ni mikubwa imepata 
Baraka zote kutoka TUCTA (Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi) na Baraza
 la Michezo la Taifa (BMT),” alisema Benjamin. 
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni