AFISA WA VIJANA WA MUUNGANO WA ODM AUWAWA JIJINI NAIROBI

Afisa wa Vijana wa Muungano wa Siasa wa ODM, amepigwa risasi jana usiku na kufa akiwa nje ya geti la nyumba yake eneo la Ruai, Jijini Nairobi.

Afisa huyo Stephen Odongo Mukabana, 42, alishambuliwa wakati akingojea kufunguliwa geti, kwa mujibu wa Mkuu wa Polisi wa Kituo cha Ruai, Kayole OCPD Ali Nuno.

Mukabana alivamiwa na watu sita, ambapo mmoja wao alikuwa na bastola ambayo alitumia kumpiga risasi kichwani na tumboni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni