FILIMBI ZAKATIZA KWA MUDA HOTUBA YA RAIS KENYATTA BUNGENI

Filimbi zimepulizwa na baadhi ya wabunge kabla ya rais Uhuru Kenyatta hajasimama kutoa hutuba yake mwaka kwa taifa bungeni.

Spika wa Bunge Justini Mururi alilazimika kuingilia kati ili kuleta utulivu na kusoma vifungu vya kanuni za bunge, hata hivyo rais Kenyatta alipoanza kuhutubia filimbi zikaibuka tena.

Kufuatia filimbi hizo wabunge Opiyo Wandayi, Millie Odhiambo, Simba Arati, John Mbadi, Gladys Wanga na Seneta Moses Kajwang waliamuriwa kutoka nje ya bunge.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni