Wananchi
 wa kijiji cha Malekichanda kilichopo katika kata ya Mang’ola  wilayani 
karatu mkoani Arusha wamelalamikia kitendo cha serekali kufungia ziwa  
Eyasi na  kusema kuwa kitendo hicho kimewafanya vijana wengi kukosa kazi
 na kinaweza kusababisha wananchi wa eneo hilo kukumbwa na baa la njaa 
kutokana na kumaliza chakula  chote ambacho walikuwa wamekihifadhii kwa 
ajili ya chakula  cha akiba akiba.
Hayo waliyasema leo wakati   Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shaka
 Hamdu Shaka alipofanya ziara yakutembela na kukagua baadhi ya miradi 
inayofanywa na  chama pamoja na kuongea na wananchi wa kata hiyo.
Walisema
 kuwa wanasikitishwa sana na kitendo cha  mkuu wa 
wawilaya  kuwasimamisha  shughuli zao za uvuvi kwani ndizo walizokuwa 
wakizitegemea  katika kujipatia kipato pamoja na chakula katika kijiji 
hicho na kata kwa ujumla.
Mmoja
 wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina Kristopher Nyato alisema 
kuwa tangu marchi 19 walizuiwakufanya shughuli zao za uvuvi katika eneo 
hilo na kupewa masaa 24 kuondoka katika eneo hilo kwakile kilichodaiwa 
kuwa eneo hilo limekubwa na ugonjwa wa kipindu pindu.
“unajua  mimi  ni
 mfanya biashara nimetokea mbali nasio mimi tu tupo wengi naninavijana 
wangu ambao nimekuja nao hapa kwa ajili ya shughuli hii ya uvuvi 
sasa  tarehe hiyo  19 mwezi wa tatu mkuu wawilaya alikuja apa na askari 
nakutupa masaa 24 tuwe tumeondoka kuhoji nini ni wakatuambia  ni 
pachafu  mara waseme kuna kipindu pindu tukawaambia kama ni pachafu 
watuache wakagoma wakasema tumesema muondoke ndiposisi  kwa kuwa 
tunaogopa nakamaunavyojua wananchi tulivyo waoga tukaondoka na 
tulivyoondoka walituambia  baada ya siku chache wangefungua lakini adi 
sasa apajafunguliwa  tunateseka sana ata vyakula vyetu vya akiba 
tumemaliza yaani apa ni tabu tu”alisema Nyato
Kwa
 upande wa mwananchi mwingine aliejitambulisha kwa jina la Wiliam Jonas 
alisema kuwa mara baada ya ziwa hilo kufungwa wamekuwa wanaishi maisha 
ya kuomba omba ,wao kama wananchi wanagawana chakula walichokuwa 
wamekiifadhi na kinakaribia kwisha na vijana wengi walikuwa wakifanya 
shughuli za uvuvi katika ziwa hilo wamekuwa wazururaji.
Akiongea na wananchi hao Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shaka
 Hamdu Shaka alisema kuwa   yeye kama katibu amesikia malalamiko yao 
naatayafanyia kazi kwa kukutana na mkuu wawilaya nakuona ni jinsi gani 
ambavyo wataweza kutatua tatizo hilo.
Gazeti hili halikuishia hapo ilibidi kumtafuta mkuu wa wilaya ya karatu Omary Kwaanq
 ili kuzungumzia tuhuma hizi nakusema kuwa kweli wamelifunga ziwa hilo 
kutokana na ugonjwa wa kipindu pindu ambao umeikumba wilaya yake .
Alisema
 kuwa mpaka sasa wilaya yake ina wagonjwa 70 wa kipindu pindu na 
wamefanya utafiti ukaonyesha wagonjwa wengi wametokea maeneo ya ziwa 
hilo.
“tumefanya
 utafiti kiukweli kwa kushirikina na mtaalamu wamagonjwa wa milipuko 
nakubaini kuwa maji yale ya ziwa yana chembe chembe za wadudu wanao 
eneza ugonjwa wa kipindu pindu hivyo tukaamua ni borakufunga ziwa ilo 
ili wananchi wasiendelee kuzurika na ugonjwa huo.
Aliongeza
 kuwa mara baada ya kuona maji yale ya ule mto yana vimelea vya ugonjwa 
wa kipindu pindu ndio maana wakaona ni bora wafunge ziwalile  ili 
wananchi wasiendele kupata ugonjwa huo hatari.
 Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka akiwa
 anaongea na wananchi wa kata ya Mang'ola hiii leo wakati alipofanya 
ziara katika kata hiyo iliopo ndani ya wilaya ya karatu mkoani Arusha
 Diwani
 wakata ya mang'ola  Lazaro Gege  akiwa anampa maelezo kwa ufupi  ya 
mradi wa matofali kaimu katibu mkuu wa vijana CCM taifa
Mwenyekiti
 wa umoja wa  vijana wa ccm Mkoa Arusha Sabaya Lengai akiwa anaongea na 
wananchi wa kata ya Mang'ola hii leo wakati wa ziara ya kaimu katibu 
mkuu wa vijana taifa 
 | 
baadhi ya wananchi wakiwa wanaendelea kufatilia mkutano huo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni