Balozi
 wa Kimataifa wa UNAIDS, Mette-Marit akizungumza na waandishi wa habari 
kuhusu kazi anazofanya kama balozi wa UNAIDS kwa kipindi cha miaka 10 
tangu aanze kazi hiyo. (Picha na Rabi Hume wa Modewjiblog)
Katika
 kuhakikisha watu wanaoishi na UKIMWI wanaishi kwa furaha bila 
kunyanyapaliwa na watu wanaowazunguka, jamii imetakiwa kuwa na mtazamo 
tofauti kwa watu wanaoishi na ugonjwa huo.
Hayo
 yalisemwa na mke wa mtoto wa mfalme wa Norway, Mette-Marit ambaye pia 
ni balozi kimataifa wa Shirika la Umoja la kupambana na HIV na UKIMWI 
(UNAIDS) wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kazi
 anazozifanya kwa UNAIDS kama balozi ambaye anazunguka maeneo mbalimbali
 duniani ili kuelimisha jamii kuhusu UKIMWI.
Mette-Marrit
 alisema kuwa watu wenye UKIMWI ni kama watu wengine hivyo wana haki ya 
kupata huduma bila kunyanyapaliwa ili waweze kuishi kwa uhuru kama watu 
wengine na ili kufanikisha hilo ni wajibu wa kila mtu kuwasaidia 
waathirika.
“Watu
 kuwa na UKIMWI sio mwisho wa maisha inatakiwa kwanza jami kuwa na 
mtazamo tofauti na inatakiwa kila mtu kusaidia mapambano ya UKIMWI sio 
jambo la mtu mmoja mmoja,” alisema Mette-Marit.
Mwenyekiti
 wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS), Dkt. Fatma Mrisho 
akizungumzia kuhusu juhudi zinazofanywa na serikali katika mapambano ya 
UKIMWI.
Nae
 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS), Dkt. Fatma 
Mrisho alisema Serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali ili 
kupambana na UKIMWI lakini pia ili kufanikisha mapambano hayo wanahitaji
 kushirikiana na taasisi ambazo zitawasaidia katika mapambano hayo.
Lakini
 pia Dkt. Mrisho amezitaka serikali za mitaa kuacha kusubiri mpaka 
serikali imepeleke pesa ndiyo wawasaidie watu wanaoishi na UKIMWI na 
hivyo waweke utaratibu wa kutumia sehemu ya mapato yao ili kusaidia 
mapambano hayo.
“Serikali
 haijalala katika mapambano tunahitaji kushirikiana na taasisi ambazo 
zinatusaidia kupunguza maambukizi mapya na tunaona Mette-Marit amekuwa 
akifanya jambo zuri anazunguka sehemu nyingi ili kusaidia kupunguza 
maamukizi mapya ya UKIMWI,” alisema Dkt. Mrisho.
Mkurugenzi mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na Ukimwi, UNAIDS nchini Tanzania, Warren Naamara akizungumzia ugonjwa wa UKIMWI.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni