
Rais
 Mstaafu wa awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete, akijiandaa kuzungumza na 
Wanafunzi na wanachama wa CCM waishio Mji wa Beijing nchini China.
 Rais
 Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete, akizungumza na wanafunzi na Wanachama wa 
CCM, waishio nchini China, wakati alipokutana nao akiwa katika ziara 
yake nchini humo.
**************************************
Na Mwandishi Wetu, Beijing China
Mwenyekiti
 wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi {CCM} na Rais mstaafu wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt Jakaya Mrisho Kikwete leo tarehe 
20th April 2016 amekutana na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wa Tawi la
 Beijing ambao ni Wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya elimu ya juu, katika 
Ukumbi wa Grand uliopo katika Makazi ya Viongozi ya Diaoyutai State 
Guesthouse jijini Beijin, nchini China.
Wakisoma
 risala yao, Wanafunzi hao kutoka vyuo mbalimbali vilivyopo Beijin na 
miji ya karibu kama vile Tianjin walimuhakikishia Mheshimiwa Dkt. 
Kikwete kuwa wao ni waaminifu na wazalendo kwa Taifa lao na kwamba wako 
tayari kurudi nyumbani na kutumia elimu zao katika kuhakikisha kuwa 
maendeleo ya kiuchumi na kijamii yanafikiwa.
Katika
 mazungumzo na Wanachama hao, Mhe Kikwete amewakumbusha jukumu kubwa 
lililo mbele yao la kujenga Chama na kulijenga Taifa la Tanzania, katika
 hotuba yake ameeleza kuwa China imefanya Mapinduzi makubwa katika 
maendeleo na kuboresha ustawi wa watu wa nchi hiyo, hivyo kuwataka 
kujifunza na kuchukua maarifa ya China na kuyatumia wakirudi nchini ili 
kufanikisha Mapinduzi makubwa ya Kiuchumi na maendeleo kwa ujumla.
 Mheshimiwa
 Kikwete na Ujumbe wake wanatarajia kutembelea Jimbo la Fu Zhou hapo 
kesho na kushuhudia maendeleo makubwa yaliyosimamiwa na Katibu Mkuu wa 
CCP na Rais wa Serikali ya watu wa China Mhe Xi Jinping, pamoja na 
kufanya mazungumzo muhimu na Viongozi wa Chama Cha Kikomunisti cha China
 {CCP} katika jimbo hilo.
 Rais
 Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete, akizungumza na wanafunzi na Wanachama wa 
CCM, waishio nchini China, wakati alipokutana nao akiwa katika ziara 
yake nchini humo.
Picha ya pamoja baada ya mazungumzo yake na wanaccm na wanafunzi wwatanzania waishio China.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni