Mkuu
 wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema ambaye alikuwa mgeni rasmi wa 
uzinduzi wa Michuano ya Shule za Sekondari Nchini (UMESETA), akipiga 
dana dana wakati wa uzinduzi huo uliofanyika Uwanja wa Uhuru Dar es 
Salaam leo.
 Wanafunzi wa shule za sekondari za mkoa wa Dar es Salaam wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Mkuu
 wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (kushoto), akikabidhi vifaa vya 
michezo kwa Shule ya Sekondari ya Azania vilivyotolewa na Kampuni ya 
Coca Cola. Kulia Ofisa kutoka kampuni ya Coca Cola wadhamini wakubwa wa 
michuano hiyo kwa mwaka 2016.
 DC
 Mjema akisalimiana na mwamuzi wa mchezo kati ya timu ya Sekondari ya 
Tirav ya Yombo na Makongo uliopigwa katika Uwanja wa Uhuru Dar es 
Salaam. Makongo ilishinda mabao 2-1.
 DC Mjema akiwasalimia wachezaji wa timu ya Tirav.
 DC Mjema akisalimiana na wachezaji wa timu ya Makongo Sekondari.
Mkuu wa Wilaya Sophia Mjema (kulia), akitoa nasaha zake kwa wachezaji hao kabla ya kuanza kucheza.
DC Mjema hapa akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya sekondari ya Tirav na viongozi mbalimbali.
DC Mjema hapa akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya sekondari ya Makongo na viongozi mbalimbali.
Hapa akiwa katika picha ya pamoja na waamuzi wa mchezo huo na viongozi mbalimbali.
Hapa mtanange ukiendelea.
Golikipa wa timu ya Tirav, Abdul Badi akiokoa moja ya hatari katika lango lake.
Wachezaji wa timu ya Makongo wakishangilia baada ya kupata bao lao la kwanza.
Na Dotto Mwaibale
MKUU 
wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema amezindua michuano ya Shule za 
Sekondari Nchini (UMESETA) katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam 
huku akisisitiza kuwa yataendelea kuwaibua wachezaji wengi chipukizi.
Akizungumza
 katika uzinduzi huo Mjema aliishukuru kampuni ya Cocacola kwa kudhamini
 mashindano hayo huku akiyaomba makampuni na wadau wengine kujitokeza 
kudhamini michezo mbalimbali.
Mashindano
 hayo yatashirikisha timu zaidi ya 40 katika mchezo wa mpira wa kikapu 
kwa vijana wa Shule za Sekondari kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini 
huku ikishirikiana na waandaaji wa michuano ya michezo ya Shule za 
Sekondari UMISETA katika kuhakikisha wanapata wachezaji wenye elimu 
kutoka mikoa yote hapa nchini.
Akizungumzia
  mashindano hayo  Meneja wa Biashara wa Coca Cola Maurice Njowoka 
alisema wameamua kuongeza mchezo ili kupanua wigo wa mashindano hayo 
hapa nchini.
Aidha
 alisema lengo la kuungana na waandaaji hao, badala ya Shirikisho la 
soka Tanzania (TFF) pekee ni kutaka kupata wachezaji sahihi, kutoka 
mikoa yote, na ambao wako katika mashule ya Sekondari.
"Hii itatusaidia kupata wachezaji sahihi wenye elimu na ambao kweli wanasoma shule za sekondari,"alisema Njowoka.
Alisema tofauti na mwaka jana, tuliwatumia TFF pekee jambo ambalo tulipata wachezaji lakini katika mazingira magumu zaidi.
Alisema
 michuano ya mwaka huu wanaimani watapata wachezaji kiurahisi kwa sababu
 UMISETA ina rekodi ya wanafuzni wanaosoma katika shule za sekondari.
Njowoka
 alisema kwa kuanzia jijini Dar es Salaam, wametoa jezi na vifaa kwa 
shule za Sekondari zilizohudhuria katika mashindano hayo.
Alisema
 baada ya Dar es Salaam, wanaelekea Mwanza, Mbeya, Arusha na Moshi kwa 
ajili ya kuzindua rasmi michezo hiyo ambayo shule zinaanza kufanya 
mazoezi kwa ajili ya kujiandaa.
Alisema
 katika udhamini wao watatumia kinywaji cha Coca Cola kwa upande wa 
soka, wakati Kikapu watatumia Sprite, lengo ni kufanikisha michuano hiyo
 safari hii kutokana na kuongeza idadi ya mchezo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni