Habari na picha na  John Nditi, Morogoro
WAZAZI na walezi wenye watoto wenye ulemavu wilayani Mvomero , mkoa wa  Morogoro wametakiwa kuwapeleka shule ili waweze kupata elimu itakayokuwa ni mkombozi wao kwa maisha yao ya baadaye katika kujiletea maendeleo yao ya kijamii na kiuchumi,  imeelezwa.
Rai
 hiyo ilitolewa na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, George 
Jackson Mbijima ,Aprili 20, 2016  wakati wa uzinduzi wa Darasa la watoto
 wenye ulemavu , katika kijiji cha Changarawe, Kata ya Mzumbe , wilayani
 humo. 
 Kiongozi
 wa Mbio za Mwenge wa Uhuru , Mbijima , alitumia fursa hiyo kuwataka 
wazazi na jamii kwa ujumla, kuwapeleka watoto wenye ulemavu katika shule
 hiyo kwa kuwa elimu pekee ndiyo itakayowakomboa.
“
 Serikali ya Tanzania imeweka mazingira mazuri ya kusoma kwa watoto wa 
makundi yote wakiwemo wenye ulemavu wa aina mbalimbali , kwani elimu 
pekee ndiyo mkombozi wao katika suala la kujitegemea siku za 
usoni...hivyo jamii itambua hilo na kuwajali watoto wenye ulemavu na si 
kuwaficha majumbani” alisema Mbijima.
Naye
 Mwalimu wa  darasa la  watoto wenye ulemavu katika shule ya Msingi ya 
Changarawe ,  Doreen Msuya, aliiomba serikali ya Wilaya, mkoa na 
Serikali kuu, kuona uwezekano wa kujenga hosteli ya watoto wenye ulemavu
 katika eneo la shule hiyo.
Msuya
 alisema , hatua hiyo itawezesha watoto wengi wanaoshindwa kufika 
kutokana na ulemavu wao waweze kuishi karibu na shule na kunufaika na 
elimu ambayo itawasaidia katika maisha yao baadae.
Hivyo
 alisema , mradi huo wa darasa la wanafunzi wenye mahitaji maalumu 
ulianzishwa mwaka 2013 baada ya kufanyika sense ya watoto wenye mahitaji
 maalumu na kubaini watoto 26 ambao kwa kipindi hicho walikauwa 
majumbani ingawa umri wa kuanza shule ulikuwa umefika.
 Msuya
 alisema , mradi huo unatekelezwa kwa kushirikiana kati ya halmashauri 
ya wilaya ya Mvomero na wanajamii wa kijiji cha Changarawe ambao hadi 
sasa wanafunzi 42 wapo darasani , kati ya hao wavulana 27 na wasichana 
15.
“
 Kupitia mradi wa darasa hili umeweza  kuibua watoto sita waliokuwa 
wamefichwa  nyumbani  ambao ni wenye ulemavu wa aina mbalimbali” alisema
 Msuya.
“
 Kuazishwa kwa darasa la watoto wenye ulemavu katika shule hii ya 
Changarawe  kumesaidia  kuibuliwa ndani ya jamii watoto wa aina hiyo 
waliokuwa  mitaani na nyumbani bila ya matumaini yeyote ya baadaye “ 
alisisitiza Mwalimu Msuya.
Akisoma
 risala kwa niaba ya wanafunzi wenzake , mwanafunzi wenye ulemavu , 
Steven Petro (14) wa darasa la tano shuleni hapo, kuanzishwa kwa darasa 
hilo kumewawezewa wao kupata elimu na hivyo kuwa na matarajio mazuri ya 
siku za usoni.
Naye
 mkuu wa wilaya ya Mvomero, Betty Mkwasa, alihimiza wazazi kuhakikisha 
watoto wanapata fursa ya kuandikishwa shule ya awali na msingi ikiwa na 
kuwandeleza hadi elimu ya juu kwa vile elimu ndiyo ufunguo wa maisha.
Mwenge
 wa Uhuru ukiwa katika wilaya ya Mvomero  ulipitia, kuzindua, kuweka 
mawe ya msingi na kuonwa  miradi  mitano ya maendeleo yenye thamani 
zaidi ya Sh  milioni 688.6 ukiwemo  wa  darasa la watoto wenye mahitaji 
maalumu.
Tayari
 Mwenge wa Uhuru umemaliza mbio zake katika Manispaa ya Morogoro, 
halmashauri ya wilaya ya Morogoro, Mvomero , Ulanga na Kilombero tangu 
ulipozinduliwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan , Aprili 18, mwaka
 huu katika uwanja wa Jamhuri wa Morogoro.
 Baadhi
 ya watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Ulanga , mkoa wa Morogoro 
wakifuatilia jambo wakati wa ugeni wa Mwenge wa Uhuru .
 Kikundi cha Wanawake cha Mvomero kikionesha bidhaa zao.
 Kiongozi
 wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa , George Jackson Mbijima akifuatana 
na Mkuu wa wilaya ya Mvomero, mkoa wa Morogoro, Betty Mkwasa  kuangalia 
bidhaa za kikundi cha wanawawake.
 Kiongozi
 wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, George Jackson Mbijima akimkabidhi 
hati kwa klabu ya wapinga rushwa ya Twikale wose  Lugono, Mwenyekiti wa 
klabu , Kondo Mahawa.
 Mgangazaji
 wa TBC Swedi Mwinyi , ( kati kati ) akiwa pamoja na mshereheshaji 
mwenzake ( kushoto) wakati wa uzinduzi wa mbio za Mwenge  wa Uhuru 2016,
 uwanja wa Jamhuri wa Morogoro.  
 Mjasilimali
 wa Kimasai  akiwa na  Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 
pamoja  na mkuu wa wilaya ya Mvomero, Betty Mkwasa.
 Mkuu 
wa Takukuru wilaya ya Mvomero, mkoa wa Morogoro, Eufrasia Kayombo ( 
kushoto) akisaini hati ya uzinduzi wa klabu ya wapinga rushwa Twikale 
wose , Lugono kilichopo wilaya ya Mvomero.
 Mkuu 
wa wilaya ya Mvomero, mkoa wa Morogoro, Betty Mkwasa akiwa ameushika 
Mwenge wa Uhuru , baaada ya kukabidhiwa na Mkuu wa wilaya ya Morogoro, 
Muhingo Rweyemamu ( hayupo pichani).
 Mkuu 
wa wilaya ya Ulanga, mkoa wa Morogoro, Christina Mndeme, ( kulia) 
akimkabidhi Mwenge wa Uhuru mkuu wa wilaya ya Kilombero, Lephy Gembe ( 
kushoto),kuanza mbio zake Aprili 22, 2016
| Wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa , wakitoka kuweka jiwe la msingi jengo la kuhifadhia dawa na vifaa tiba katika hospitali ya wilaya ya Ulanga. | 
 Mmoja
 wa wakimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa akiwa ameubeba Mwenge wa Uhuru, 
baada ya kuvuka katika kivuko cha Mv Kilombero 11 kutokea wilaya ya 
Ulanga. (1)
Mwanafunzi
 mwenye ulemavu wa viungo, Steven Petro  wa darasa la tano shule ya 
Msingi Changarawe, wilaya ya Mvomero akisoma risala. 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni