Mgakuzi wa Vyakula kutoka Mamlaka a Chakula na Dawa, Dk Itikija Mwanga (kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri
 wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba na Waziri wa Afya, Maendeleo
 ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu walipotembelea 
machinjio hayo, Vingunguti jijini Dar es Salaam . 
WIKI 
moja baada ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuyafunga machinjio ya 
Ng’ombe na Mbuzi Vingunguti jijini Dar es Salaam kwa uchafu na 
kusababisha bei ya nyama kupanda, serikali imeitaka Halmashauri ya 
Manipaa ya Ilala kufanya marekebisho ya haraka ili uchinjaji uanze mara 
moja.
 Kaimu
 Mkuu wa Idara ya Mifugo katika Manispaa ya Ilala, Msongo Songoro 
(kulia)  akitoa ufafanuzi juu ya marekebisho yaliyoanza kufanyika 
machinjioni hapo wakati Waziri wa 
Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba na Waziri wa Afya, Maendeleo ya 
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu walipotembelea. 
 Waziri
 wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba akizungumza jambo. Kushoto 
ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Vingunguti, Omary 
Kumbilamoto. 
 Moja 
ya vitu vilivyo sababisha machinjio hayo kufungwa ni pamoja na mabomba 
yote ya karo za kusafishia utombo na nyama kukosa maji. Hii ilieklezwa 
na wasimamizi kuwa kila zinapowekwa koki huibiwa. 
 Mbunge
 wa jimbo la Segerea Bona Kaluwa akipita katika moja ya maeneo ya 
machinjio hayo ambayo ni machafu na nyama huuzwa humo na kuhatarisha 
afya za walaji. Aidha Mbunge huyo alisema kuwa kuna vitendo vichafu 
hufanyika machinjioni hapo nyakati za usiku. 
 Waziri
 wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu 
(wapili kulia) akizungumza na Mkaguzi wa Chakula kutoka Mamlaka ya 
Chakula na Dawa (TFDA), Dk Itikija Mwanga (kulia) wakati yeye na Waziri 
wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba (hayupo pichani) 
walipotembelea Machinjio ya Vingunguti Dar es Salaam jana. Kushoto ni 
Naibu Meya wa Ilala na Diwani wa Vingunti, Omary Kumbilamoto na wapili 
kulia ni Mbunge wa Segerea, Bona Kaluwa
 mawaziri hao wakiendelea na ziara yao ya kukagua mazingira ya machinjio hayo. 
 Hapa 
ni sehemu ya kuhifadhia nyama na kuuzwa ambayo nayo imelalamikiwa kuwa 
vyuma vyake vuina kutu na pia ni makosa kuuza nyama katika machinjio. 
 Kutu ilivyo katika vyuma hivyo. 
Waziri
 wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu na 
 Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba wakijadiliana jambo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni