PAPA WEMBA ALIKUWA ANATAKA KUFARIKI AKIWA JUKWAANI

Promota wa tamasha la Papa Wemba, Salif Traore, maarufu kama A'Salfo, amesema Papa Wemba alimuambia kuwa angependa kufa akiwa jukwaani, katika maongezi yao waliyoyafanya kwa njia ya simu wiki mbili kabla ya kifo chake.

Papa Wemba mwanamuziki maarufu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo alifariki dunia Jukwaani nchini Ivory Coast wakati akitumbuiza baada ya kuanguka hafla na kisha baadaye kuelezwa kuwa amefariki dunia.
Papa Wemba akishambulia jukwaa pamoja na mnenguaji wake kabla ya kuanguka na kufariki dunia
                   Papa Wemba akionekana mwenye afya njema wakati akitumbuiza
Papa Wemba akifurahi na mashabiki waliokuwa wakishuhudia onyesho hilo ambalo ndio la mwisho kabla ya kuaga dunia
Wanamuziki wa bendi ya Papa Wemba wakiwa wamemzingira baada ya kuanguka chini

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni