WATU WASIOJULIKANA WATUMIA NAMBA YA SIMU YA MBUNGE WA JIMBO LA MOSHI MJINI KUTAPELI.

TANGAZO KWA UMMA.

Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini Jafary Michael (Chadema) anatoa tahadhari kwa umma ya kuwa kuna baadhi ya watu wenye nia mbaya wanatumia namba yake ya simu ya mkononi ya mtandao wa Vodacom kufanya utapeli .

Watu hao wamekuwa wakituma ujumbe mfupi (SMS) kwa watu mbalimbali kwa lengo la kutapeli wakiomba kutumiwa fedha .

Wakati akishughulikia suala hilo katika vyombo vya dola ametoa ombi kwa yeyote atakayepata ujumbe huo kuupuza na kutoa taarifa kwa yeyote atakaye fikwa na kadhia hiyo.

Ukipata ujumbe huu mfahamishe na mwenzako.

Imetolewa na :
Japhary Michael
Mbunge wa Moshi mjini

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni