MVUA KUBWA YASITISHA USAFIRI WA NDEGE NA TRENI NCHINI INDIA

Mvua zilizoanza upya katika mji wa Chennai kusini wa India zimesababisha mafuriko makubwa na kusababisha ndege na treni kusitisha usafirishaji na mamia kuachwa bila umeme.

Jeshi la India limepelekwa katika mkoa huo kuwaokoa maelfu ya watu waliokwama baada ya mvua kunyesha kwa siku mbili.

Watu wapatao 188 wamethibitishwa kufa kutokana na mafuriko katika jimbo la Tamil Nadu tangu mwezi uliopita.
                   Wanafamilia wakimsaidia kumuokoa mwanamke mwenye ulemavu
      Wananchi wakiwa kwenye boti huku polisi wakilisukuma kuwavusha kwenye mafuriko.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni