Mmiliki wa Facebook, Mark Zuckerberg
pamoja na mkewe Priscilla Chan wamesema watagawa hisa zao asilimia 99
kwa ajili ya kusaidia wenye mahitaji, wakati wakitangaza kuzaliwa kwa
mtoto wao wa kike Max.
Mark Zuckerberg ametoa tangazo hilo
katika barua kwa mtoto Max aliyoiweka kwenye ukurasa wake wa
Facebook.
Wamesema wanatoa hisa hizo kwa
Taasisi ya Chan Zuckerberg kwa kuwa wanataka kuifanya dunia kuwa
sehemu nzuri kwa Max kukulia. Msaada huo kwa sasa unafikia dola
bilioni 45.
Binti Max alizaliwa wiki iliyopita,
hata hivyo wanandoa hao waliamua kutangaza kuwa wamepata mtoto hapo
jana.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni