MWANARIADHA OSCAR PISTORIUS ATIWA HATIANI KWA MAUAJI, KUBADILISHIWA KIFUNGO

Mwanariadha Oscar Pistorius ametiwa hatiani kwa kosa la mauaji baada ya mahakama ya rufaa nchini Afrika Kusini, kutengua hukumu ya awali ya kuuwa bila ya kukusudia.

Pistorius alimuua mpenzi wake mwanamitindo Reeva Steenkamp mwezi Februari 2013, kwa kumfyatulia risasi mara nne akiwa ndani ya choo ambacho mlango wake ulifungwa.

Kwa sasa Pistorious ambaye ni mwanariadha mlemavu wa miguu yote miwili yupo anatumikia kifungo cha nyumbani, baada ya kukaa jela mwaka mmoja kati ya miaka mitano aliyohukumiwa.

Pistorius sasa atarejea mahakamani kubadilishiwa adhabu na kuwa ya mauaji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni