WANAJESHI WA CAMEROON WAWAKOMBOA WATU 900 KUTOKA KWA BOKO HARAM

Vikosi vya jeshi la Cameroon vimewaokoa watu 900 waliokuwa wakishikiliwa na kundi la Boko Haram, Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo ametangaza.

Waziri huyo Joseph Beti Assomo amesema vikosi hivyo pia vimewauwa wapiganaji wa kundi hilo 100 hadi kufikia mwisho wa mwezi Novemba.

Hata hivyo hakuna uthibitisho huru kuhusiana na operesheni hizo za jeshi la Cameroon katika eneo la kando la mkoa wa Kaskazini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni