BASI LA SIMBA MTOTO LAGONGANA NA LORI, ABIRIA KADHA WAHOFIWA KUFA

Taarifa zilizotufikia zinasema watu kadhaa wanahofiwa kufa na wengine kujeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Simba Mtoto lililokuwa linasafiri kutoka Tanga kuelekea jijini Dar es Salaam kugongana na lori la mizigo leo asubuhi. 

Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema juhudi kubwa zinaendelea kufanywa na jeshi la polisi kwa kushirikiana na wananchi kuwanasua abiria ambao bado wamenasa ndani ya basi hilo.

Kwa mujibu wa mashuhuda wamesema kuwa magari hayo yaligongana uso kwa uso. Tutawaletea taarifa zaidi kadiri zitakavyotufikia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni