KATIBU MKUU MAMBO YA NDANI YA NCHI AZINDUA BODI YA CHUO CHA UHAMIAJI CHA KIKANDA (TRITA) MJINI MOSHI

Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Victoria Lembeli akizungumza na wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) katika hafla fupi ya uzinduzi wa Bodi hiyo iliyofanyika mjini Moshi. Watatu kulia meza kuu ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira. Kushoto ni Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu, wapili kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo, Kinemo Kihomano.na kulia ni Kamishna wa Chuo hicho, John Choma.
Mkufunzi Mkuu wa Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) mjini Moshi, Erasmi Francis akimuonyesha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kushoto) na wajumbe wa Bodi ya Chuo hicho, kamera inayotumika kuchukua kumbukumbu za usalama kwa ajili ya watu wanaopita katika mipaka ya nchi. Wapili kushoto ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Victoria Lembeli. Watatu kulia ni Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu, na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho, Kinemo Kihomano (Wasita kushoto)

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (katikati waliokaa), Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Victoria Lembeli (wapili kushoto waliokaa), Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA), mara baada ya Katibu Mkuu huyo kuzindua Bodi hiyo mjini Moshi. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni