POLISI UGANDA WAMKAMATA KIONGOZI WA UPINZANI ANAYEWANIA URAIS DK. KIZZA BESIGYE

Polisi nchini Uganda imemkamata kiongozi wa upinzani anayewania urais Dk. Kizza Besigye akiwa kwenye moja ya barabara kuu Jijini Kampala.

Mashahidi wamesema polisi walifyatua mabomu ya machozi kuwasambaza mamia ya wafuasi wa Dk. Besigye waliokuwa wakimsindikiza.

Dk. Besigye ni miongoni mwa wagombea urais saba wanaowania kumg'oa madarakani rais Yoweri Museveni ambaye ameiongoza Uganda kwa miaka 30, katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Alhamisi wiki hii.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni