Aliyekuwa mwenyekiti wa IPC Daud Mwangosi (kushoto) akihojiwa na 
mzee wa matukio daima Bw Francis Godwin  ambaye alikuwa ni katibu 
msaidizi wa IPC juu ya wanahabari kudumisha umoja na mshikamano wakati 
wa uhai wake.
Mwandishi
 wa habari wa Chanel Ten mkoa wa Iringa na Mwenyekiti wa cha chama cha 
waandishi wa habari mkoa wa Iringa Daud Mwangosi tarehe Kama ya leo 
miaka mitatu iliyopita aliuwawa  katika vurugu za Polisi  na wafuasi wa 
Chadema katika kijiji cha Nyololo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa .
Mwanahabari
 huyo Daud Mwangosi aliuwawa majira ya saa 10 jioni katika ofisi za 
Chadema Nyololo huku askari mmoja akijeruhiwa vibaya kwa risasi .
Kabla
 ya kuuwawa kwa mwanahabari huyo mabomu yaliweza kupigwa eneo hilo 
kuwatawanya wafuasi hao wa Chadema ambao walikuwa wakigoma kutawanyika 
eneo hilo na kuamua kukaa chini kuwa haapo tayari kuondoka katika ofisi 
yao.
Chanzo
 cha mwanahabari Mwangosi kuuwawa kilitokana na kukamatwa kwa mwandishi 
wa habari wa gazeti la Nipashe mkoa wa Iringa Godfrey Mushi na hivyo 
mwanahabari huyo kkutaka kuhoji polisi sababu ya kukamatwa kwa 
mwanahabari huyo ndipo askari hao walipoanza kumshambulia kwa kichapo na
 baadae mlio kama wa bomu ulisikika eneo hilo na mwandishi huyo na 
askari mmoja waliaguka chini .
Ndani
 ya dakika tano ilisikika sauti kutoka kwa askari huyo kuwa afande 
nimekufa ndipo walipomchukua na kumpeleka Hospitali ya wilaya ya Mufindi
 huku mwili wa mwanahabari huyo ukipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti .
Katika
 vurugu hizo zilizodumu kwa takribani dakika 30 kwa askari na wafuasi wa
 Chadema kurushiana mawe kwa mabomu zaidi ya magari matano ya Chadema na
 ya wananchi yameharibiwa huku watu kadhaa wamejeruhiwa na mwanahabari 
mmoja Godfrey Mushi akijeruhiwa vibaya.
Hii ni taarifa ya Jeshi la polisi kabla ya tukio kwa vyombo vya habari
JESHI
 la polisi mkoa wa Iringa limesema limezuia mikutano ya vyama vya siasa 
kwa vyama vyote na sio kwa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) 
pekee hivyo laonya vyama vyote kutii sheria bila shuruti.
Hata
 hivyo jeshi hilo la Polisi limesema kuwa halifanyi kazi kwa matakwa ya 
chama chochote cha siasa na kuwa si kweli kama wanavyodai viongozi wa 
Chadema kuwa jeshi la polisi linatumiwa na chama cha mapinduzi (CCM) 
kuzuia mikutano hiyo.
Kamanda
 wa polisi wa mkoa wa Iringa Michael Kamuanda ametoa kauli hiyo leo 
ofisini kwake alipozungumza na waandisha wa habari kuhusu zuio la 
mkutano wa Chadema uliopangwa kuanza leo katika wilaya ya Mufindi.
”
 Nawatangazia wanasiasa na vyama vyote vya siasa pamoja na wananchi wa 
mkoa wa Iringa kuwa hakutakuwa na mikutano ya kisiasa kutokana na 
shughuli za sensa zinazoendelea ….hivyo basi nawaomba wananchi wote 
kutoshiriki mikutano yoyote ya kisiasa itakayoitishwa na wanasiasa 
“alisisitiza
Kuwa
 mikutano hiyo imezuiliwa kwa kipindi hiki cha sensa kilichoongezwa hadi
 hapo tamko litakapotolewa tena na msajili wa vyama vya siasa John 
Tendwa kama alivyokwisha kutoa tamko la kuzuia shughuli hizo za vyama 
vya siasa kwa kipindi hiki cha sensa.
“Wananchi
 wote wa mkoa wa Iringa mnaombwa kutii sheria bila shuruti hii ni amri 
….nawaombeni sana wananchi kutodanganywa na wanasiasa kwa kuvunja sheria
 “aliongeza kamanda huyo wa polisi.
Hata
 hivyo alisema kuwa kimsingi zoezi la sensa lilipaswa kuhitimishwa 
Septemba mosi mwaka huu ila kutokana na serikali kuongeza muda wa zoezi 
hilo bado jeshi hilo la polisi linazingatia maagizo ya Msajili wa vyama 
vya siasa kama alivyoyatoa kwa jeshi hilo.
Kamanda
 Kamuanda alisema kuwa jeshi hilo la polisi wala msajili wa vyama vya 
siasa hajazuia vyama vya siasa kuendelea na vikao vyao vya ndani kwa 
kipindi hiki na kuwa hata Chadema wakiwa mkoani Iringa wameendelea 
kufanya vikao vyao vya ndani katika kata mbali mbali za mkoa wa Iringa 
na hakuna mtu aliyewazuia kuendelea kufanya hivyo.
Majibu ya Dkt Slaa
Wakati
 jeshi la polisi likipinga shughuli hizo za vyama vya siasa kufanya 
mikutano ya hadhara katibu mkuu wa Chadema Taifa Dkt Willbroad Slaa 
ameibuka na kusema kuwa chama chake kitaendelea na mikutano kama 
kilivyojipangia na kuwa wapo tayari kwa lolote litakalojitokeza .
Dkt
 Slaa alisema kuwa walivumilia mara ya kwanza walipozuiwa mikutano hiyo 
mkoani Iringa na kuvuta subira hadi jumamosi zoezi hilo lilipomalizika 
sasa anashangazwa kuona jeshi hilo likiendelea kuzuia mikutano hiyo 
tena.
“Tumemsikiliza
 kamishina wa sensa Hajati Amina Mrisho Said kuwa hadi sasa watu 
asilimia 95 wameandikishwa huku akiwata wale ambao bado kuwapigia simu 
wenyeviti wa mitaaa na vijiji ili wakaandikishwe na makarani wa sensa 
….sasa jeshi la polisi linataka kutuambia kuwa hao watu asilimia 5 
waliobaki wapo Iringa peke yake hadi wakazuia mikutano yetu? tunasema 
hatutakubali tutaendelea na mikutano yetu kama kawaida hatupotayari 
kabisa kusubiri hadi tarehe nane” alisema Dkt Slaa.
Pia
 alisema kuwa kama ni uzalendo sasa umefika kikomo na kuwa wataendelea 
na ratiba zao za mikutano kama ilivyopangwa na watapambana kwa lolote .
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni