RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AMJULIA HALI MUFTI NA SHEIKH MKUU WA TANZANIA PAMOJA NA KUFANYA UKAGUZI WA KUSHTUKIZA KATIKA WODI YA WAZAZI YA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI
posted on
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali Mufti
na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir ambaye amelazwa kwenye
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu.
Mufti
na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir akimuombea Dua Raiswa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli mara baada ya Rais Dkt. Magufuli kumjulia hali Hospitalini hapo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiombewa Dua na
ndugu na jamaa mbalimbali ambao walifika Muhimbili kuwaona wagonjwa wao.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akielekea katika
Wodi ya Wazazi kufanya ukaguzi wa ghafla mara baada ya kuwasili akitokea
Dodoma.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na
wagonjwa waliolazwa katika Wodi ya Wazazi na amewahidi kutatua kero zao ndani
ya muda mfupi ujao.PICHA NA IKULU
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni