ABIRIA WA NDEGE AIBUA UGOMVI ANGANI BAADA YA KUMKOJOLEA ABIRIA MWENZAKE

Abiria mmoja amedaiwa kumkojolea msafiri mwenzake, na kusababisha kuibuka kwa ngumi wakati ndege ya Meditarranee ikiwa angani, vyombo vya Ufaransa vimesema.

Ndege hiyo ilikuwa angani kutokea Jiji la Algiers nchini Algeria kwenda Ufaransa wakati ugomvi huo ulipoibuka angani majira ya mchana na kulazimika kutua Lyon.

Abiria wameelezea tukio kuwa lilikuwa ni la kushtua wakati mwanaume asiyenashati aliyedaiwa kumkojolea abiria mwenzake akidhiditiwa na wahudumu wa ndege.

Imeelezwa kuwa abiria huyo alifanya kitendo hicho kutokana na kupandwa na hasira kutokana na kutokunywa kileo ama kuvuta sigara angani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni