Jaji
 Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman akimshukuru Rais wa Jamhuri
 ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kwa kutimiza ahadi yake
 ya kuipatia Mahakama kiasi cha shilingi Bilioni 12.3 zitakazotumika  
katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo uboreshaji 
wa miundombinu ya Mahakama na ujenzi wa Mahakama mpya katika maeneo 
mbalimbali nchini. Kulia ni Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison 
Mwakyembe na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (kushoto).
Waziri
 wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe (wa pili kutoka kushoto) 
akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa Habari kuhusu Serikali kuendelea 
kushirikiana na Mahakama ya Tanzania ili kuwezesha ufanisi wa shughuli 
zake.
Na. Aron Msigwa – MAELEZO
Jaji
 Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman amemshukuru Rais wa Jamhuri
 ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kwa kutimiza ahadi yake
 ya kuipatia Mahakama kiasi cha shilingi Bilioni 12.3 alizoahidi wakati 
wa maadhimisho ya Siku ya Sheria Februari 4, 2016 jijini Dar es salaam.
Amesema
 Fedha hizo zitatumika  katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya 
maendeleo ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ya Mahakama na ujenzi wa 
Mahakama mpya katika maeneo mbalimbali nchini.
Akitoa
 shukrani hizo leo jijini Dar es salaam Mhe.Othman amesema kuwa kwa mara
 ya kwanza tangu mwaka 2012 Mahakama imepata asilimia 100 ya fedha zote 
za Maendeleo zilizokasimiwa na Bunge kwenye Bajeti yake ya mwaka 
2015/2016.
Amesema 
 kupatikana kwa fedha hizo ambazo ni za Maendeleo kutasaidia kufufua 
miradi ya ujenzi iliyosimama, kufufua Mahakama ambazo zilikua hazifanyi 
kazi kwa sababu ya uchakavu na kuipatia Mahakama fursa zaidi ya kutoa 
huduma bora kwa wananchi kwa kuwasogezea huduma za Haki karibu katika 
maeneo wanayoishi.
Mhe.Othman
 ameeleza kuwa kwa kipindi cha bajeti za miaka 3 mfululizo kuanzia mwaka
 2012 /2013 hadi 2014/2015  Mahakama ilikua ikipokea fedha pungufu ya 
kiasi kilichopangwa katika Bajeti hali iliyochangia kuzorota kwa 
shughuli za Mahakama.
”
 Kwa mara ya kwanza Mahakama tumepata asilimia 100 ya Bajeti yetu ya 
mwaka 2015/2016 kutoaka Serikalini, mwaka 2012/2013 tulipata shilingi 
bilioni 26.9 ikiwa ni pungufu ya bajeti yetu kwa asilimia 78, mwaka 
2013/2014 tukapata Bilioni 42.7 pungufu kwa asilimia 82 na mwaka 
2014/2015 tulipewa shilingi  bilioni 41.5 ambayo ni pungufu kwa asilimia
 92 “
Akizungumzia
 miradi ya ujenzi wa majengo mapya ya Mahakama amesema kuwa tayari 
Mahakama ina michoro ya ramani za majengo yatakayojengwa katika maeneo 
mbalimbali ambayo hayakuwa na huduma hiyo ikiwemo mikoa 12 kati ya 25 
ambayo haina Mahakama Kuu, wilaya 22 kati ya 133 ambazo hazina Mahakama 
za Wilaya pamoja na kuongeza Mahakama za Mwanzo ambazo ziko 976 kufikia 
kata zote 3,957.
Kuhusu 
 Mradi wa ujenzi wa  jengo la Makao Makuu ya Mahakama utakaofanyika 
katika uwanja wa Chimala jijini Dar es salaam amesema  utahusisha  
maeneo mbalimbali ya utoaji huduma za Kimahakama na kuongeza kuwa  
Mahakama itajenga  jengo lenye viwango kwa kuwatumia Wakandarasi  na 
wataalam wa kitanzania watakaojenga  Mahakama nzuri na yenye viwango kwa
 gharama  nafuu.
“Mahakama
 tutatoa kipaumbele kwa wataalam wetu wa ndani ili waweze kutujengea 
Mahakama zetu, tunalenga kuwafikishia huduma zetu katika maeneo 
wanayoishi  tunao mfano mzuri wa Mahakama ya mwanzo ya Dumila iliyoko 
Morogoro, Mahakama hii imejengwa kijijini ni ya kisasa” Amesisitiza 
Mhe.Othman.
Kwa
 upande wake Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe amesema 
kuwa Serikali itaendelea  kushirikiana na Mahakama ya Tanzania ili 
kuwezesha ufanisi wa shughuli zake kwa kuhakikisha kuwa kiwango cha 
fedha za Bajeti kinachopitishwa kwa ajili ya kuhudumia shughuli za  
Mahakama kinafika kwa wakati.
Akizungumzia
 kuhusu uanzishwaji wa Mahakama ya Mafisadi, amesema uanzishwaji wake 
uko katika hatua nzuri na wakati ukifika wananchi watataarifiwa kama 
ilivyoahidiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuungwa 
mkono na Mahakama ya Tanzania.
Naye
 Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip  Mpango, akizungumzia fedha za 
Maendeleo zilizotolewa  na Mhe.Rais amesema kuwa lengo la ahadi ya Rais 
kwa Mahakama ilikua ni kuhakikisha Haki inapatikana kwa wananchi kwa 
Wakati na kwamba miongoni mwa vitu vilivyokua vikichelewesha haki kwa 
watanzania walio na mashauri Mahakamani ni ukosefu wa fedha na uchakavu 
wa miundombinu.
Amesema
 Serikali inaendelea kujenga uwezo wa kifedha ili kuimarisha huduma 
katika mihimili yote ikiwemo Bunge na Mahakama huku msisitizo ukiwekwa 
katika kukusanya mapato ya ndani.
“Kwa
 kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tuna dhamira ya dhati 
ya kukusanya mapato ya ndani ili kujenga uwezo wa Serikali tutawabana 
wote waliokuwa wanakwepa kulipa kodi na hili tutalisimamia kikamilifu”
Amesema
 utoaji wa Haki ni moja ya ukuzaji wa maendeleo ya nchi na kuongeza kuwa
 Mahakama ya Tanzania inafanya kazi nzuri pamoja na ufinyu wa bajeti 
yake.



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni